• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKURUGENZI SONGEA DC, AWATAKA WAKUU WA DISHENI NA VITENGO KUTENGA BAJETI ZITAKAZOENDA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Tarehe ya Kuwekwa: February 7th, 2024


Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Songea Mwl. Neema Maghembe, amewataka Wakuu wa Divisheni na Vitengo kutenga bajeti zitakazoenda kutatua kero za wananchi kwa kutazama vipaumbele vya Serikali lakini pia katika kila Idara kuangalia namna gani Idara inajihusisha na jamii kwa kuweka mikakati itakayopunguza malalamiko kwa wananchi.

“ Niwasihi wakuu wa Divishen na Vitengo, kwa sasa ndo tupo kwenye maandalizi ya bajeti ya 2024/2025, hivyo basi huu ndo wakati sahihi wa kutengeneza bajeti zenu mkizingatia mahitaji ya wananchi wetu. Mhe Rais anafanya kazi kubwa sana kuhakikisha wananchi wanapata maisha bora, hivyo tumuunge mkono ili kuhakikisha dhamira yake kwa wananchi tunaitekeleza”

Mwl. Neema ameyasema hayo katika Mkutano maalumu wa Baraza la Wafanyakazi ambalo lilikutana kwa ajili ya kujadili na kupitisha Rasimu ya mpango wa Bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka  2024/2025, ambao ulifanyika tarehe 06/02/2024 katika ukumbi wa Halmashauri iliopo kijiji cha Lundusi- Peramiho

Halmashauri ya Wilaya ya Songea, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 inakasimia kukusanya na kutumia kiasi cha TZS 28,766,811,612.00 ikiwa  TZS 16,127,854,000 ni Mishahara, TZS 1,120,508,000.00 ni fedha kwwa ajili ya matumizi mengine kutoka serikali kuu (OC), Tshs 8,943,963,200.00 ni fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo  ikiwa ( Tshs 4,695,638,000.00  fedha za ndani ( Serikali kuu), Tshs 3,841,364,000.00 fedha za nje ( Wafadhili) na Tshs 406,961,200.00 fedha za utekelezaji wa maendeleo kutoka Mapato ya ndani ya halmashauri)

Halmashauri inakadiria kukusanya na kutumia kiasi cha TZS 2,574,486,412.00 kutoka makusanyo ya mapato ya ndani ikiwa TZS 2,034,806,00 ni mapato halisi, TZS 539,680,412.00 ni mapato lindwa  ambapo  kiasi cha TZS. 1,627,844,800.00 ni fedha kwa ajili ya matumizi ya kawaida sawa na asilimia 80 na kiasi cha TZS 406,961,200.00 ni fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo sawa na asilimia 20 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Aidha katika fedha za matumizi mengine katika mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri  ya Wilaya ya Songea inakusudia kutumia kiasi cha Tshs 1,576,250,000.00 kulipa stahiki mbalimbali za waheshimiwa madiwani na watumishi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa