• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MIKAKATI WA KUBORESHA MAPATO YA HALMASHAURI WAPITISHWA SONGEA DC

Tarehe ya Kuwekwa: September 19th, 2024



Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Songea, limekaa jana, ambapo pamoja na mambo mengine, wamepitisha mikakati ya kuboresha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri, ambapo kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango imejipanga kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa ushuru na kuhakikisha mazingira bora kwa wakusanyaji


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Songea limefanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, likiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Menans Komba, huku likihudhuriwa na madiwani kutoka kata zote 16 za Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

.


Kikao hicho pia kilipitisha taarifa mbalimbali kutoka kamati za kudumu za halmashauri, ambazo ni Kamati ya Elimu, Afya na Maji; Kamati ya Kudhibiti UKIMWI; Kamati ya Nidhamu na Maadili; Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira; na Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango. Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ilionekana kuvutia zaidi hisia za wajumbe wa Baraza kwa kujadili mbinu mpya za kuongeza mapato ya Halmashauri, ikiwa ni pamoja na kuboresha vituo vya ukaguzi (mageti) ili kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unafanyika kwa ufanisi mkubwa.

ukaguzi (mageti) ili kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unafanyika kwa ufanisi mkubwa.

Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Menans Komba, alieleza kuwa halmashauri imeanza mchakato wa kuboresha vituo hivyo kwa kujenga mageti imara badala ya yale ya awali ya muda. "Tumeamua kujenga mageti thabiti ambayo yatawawezesha wakusanyaji wa ushuru kufanya kazi zao katika mazingira salama, hata wakati wa mvua au upepo. Kwa maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma ya umeme, tumeweka mpango wa kutumia nishati ya sola ili wakusanyaji waweze kuchaji mashine za POS na kuendelea na kazi zao bila kikwazo," alieleza Mhe. Komba.

Aidha, alitoa shukrani kwa madiwani kwa kuwa na uzalendo wa hali ya juu katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ndani ya kata zao. Alibainisha kuwa madiwani wamekuwa mstari wa mbele kuripoti udanganyifu unaoweza kuhujumu mapato ya Halmashauri.

"Napenda kuwashukuru kwa namna ambavyo mmekuwa makini katika kata zenu. Mmeonyesha uzalendo mkubwa kwa kutoa taarifa pale mnapohisi kuna udanganyifu katika ukusanyaji wa mapato. Hii ni hatua kubwa sana katika kuimarisha maendeleo ya Halmashauri yetu. Tutaendelea kufanya kazi kwa kushirikiana kama timu moja kwa ajili ya maendeleo," aliongeza Mhe. Komba.

Kikao hicho kilimalizika kwa madiwani kuazimia kushirikiana na kamati za Halmashauri katika kufanikisha malengo ya kuongeza mapato, huku viongozi wa Halmashauri wakiweka msisitizo katika kuimarisha uwazi na uwajibikaji kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa