• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MHESHIMIWA Menasi azindua maadhimisho ya siku ya Wazee duniani

Tarehe ya Kuwekwa: September 28th, 2022

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menasi Komba amezindua maadhimisho ya siku ya wazee duniani tarehe 27 Septemba 2022 ambayo kilele cha maadhimisho hayo ni tarehe 1 Octoba 2022.

Uzinduzi huo umefanyika katika Kata ya Peramiho Kijiji cha Peramiho A ukumbi wa Mkuwa Wilaya ya Songea.

Akizungumza katika uzinduzi huo amewataka Viongozi na wataalamu waunde mabaraza ya wazee kuanzia ngazi ya Kitongoji kwaajili ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wazee kwa haraka.

Aidha amesisitiza wazee waendelee kupewa kipaumbele katika vituo vya kutolea huduma za afya na dhana ya wazee kwanza iweze kuimarishwa Zaidi.

‘’Sisi kama Halmashauri tunawajali sana wazee hivyo tunawaahidi kutatatua changamoto zote zinazowakabili na tunampango wa kutengeneza Sheria za mtoto kumtunza mzazi hiyo yote ni kuhakikisha mnaishi katika mazingira mazuri’’, amesisitiza Mhe.Menasi.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe ambae amewakilishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Zawadi Nyoni amewashauri wazee wanawake wajiunge katika vikundi vya wanawake ili waweze kupata mikopo na kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Nae Mwenyekiti wa baraza kuu la wazee Mkoa wa Ruvuma Elenzian Nyoni amewapongeza wazee kwa kushiriki kikamilifu Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Pia ametoa rai kwa wazee kuendelea kujitokeza kwa Wingi katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kupata chanjo ya Korona.

Wakizungumza wazee wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwatatulia changamoto zinazokabiliwi ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama.

Pia wamewashukuru Viongozi wa Chama wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mheshimiwa Menace Komba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndugu Neema Mghembe na Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe.Pololet Mgema.

Katika maadhimisho hayo yalisindikizwa na maonesho ya Kilimo cha uyoga pamoja na upimaji wa magonjwa ya sukari na presha kwa wazee.

Kauli mbiu ni Ustahimilivu na mchango wa Wazee ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Imeandaliwa na Bahati Nyoni,

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Septemba 28, 2022.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KULA YAMEANZA SONGEA DC

    April 29, 2025
  • MHE . JENISTA MHAGAMA AZINDUA MADARASA 27 NA VYOO MATUNDU 44, SONGEA DC

    March 16, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa