• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Mhe. Kapinga Aongoza Baraza la Madiwani na Kupitisha Taarifa ya Hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Tarehe ya Kuwekwa: August 31st, 2024

Mhe. Kapinga Aongoza Baraza la Madiwani na Kupitisha Taarifa ya Hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024


Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mhe Simon Kapinga, ameongoza kikao muhimu cha Baraza la Madiwani kilichofanyika leo, tarehe 30 Agosti 2024, katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea. Kikao hiki kilihudhuriwa na Madiwani pamoja na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri. Lengo kuu la kikao hicho lilikuwa ni kupokea na kupitisha taarifa ya hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2023/2024.


Kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa ya mwaka 1982, kifungu namba 4, kama ilivyorekebishwa mwaka 2000, Halmashauri zote nchini zinatakiwa kufunga hesabu na kuziwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kabla ya tarehe 31 Agosti ya kila mwaka. Mabadiliko haya yametokana na marekebisho ya waraka wa Hazina uliotolewa ili kuhakikisha kuwa hesabu za mwaka wa fedha zinakamilika na kuwasilishwa mapema, tofauti na utaratibu wa awali wa kuwasilisha hesabu hizo kabla ya tarehe 30 Septemba ya kila mwaka. Waraka huu mpya unalenga kuboresha uwazi na uwajibikaji wa fedha za umma.


Taarifa ya hesabu iliyopitishwa na Baraza la Madiwani imeonyesha mtiririko mzuri wa mapato na matumizi ya halmashauri. Kulingana na taarifa hiyo, Halmashauri ilianza mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2024 ikiwa na salio la TSh 2,594,074,952.00. Jumla ya mapato kwa mwaka huo wa fedha pamoja na salio la awali yalifikia TSh 36,786,049,740.00, huku matumizi yote kwa mwaka huo yakiwa ni TSh 31,532,325,901.00. Hivyo, salio/bakaa lililokuwepo benki kufikia tarehe 30 Juni 2024 lilikuwa TSh 5,253,723,839.00.


Akizungumza baada ya kupitishwa kwa taarifa hiyo, Mhe. Kapinga aliwapongeza Madiwani kwa kazi nzuri ya kusimamia mapato na matumizi ya Halmashauri. Aidha, aliwataka kuendelea kuwa mabalozi wazuri katika kata zao, hususan wakati huu ambapo nchi inajiandaa kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Alisisitiza umuhimu wa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.


“Filimbi imepigwa kutuamsha sasa, kwamba wakati umefika,” alisema Mhe. Kapinga. “Ni jukumu letu kama viongozi kuhakikisha tunawatia moyo wananchi wetu ili wajitokeze kwa wingi kujiandikisha na hatimaye kupiga kura kwa amani. Hii itasaidia kuchagua viongozi bora watakaoweza kutumikia wananchi kwa ufanisi na kuleta maendeleo ya kweli katika jamii zetu.”


Kikao hicho pia kilijadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya Halmashauri, ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa mapato ya ndani, na mikakati ya kuboresha huduma kwa wananchi. Madiwani walisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha kuwa Halmashauri inaendelea kusonga mbele na kufikia malengo yake ya maendeleo.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YATINGA KWA KISHINDO UMISETA TAIFA

    June 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa