• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MATUMIZI YA LISHE ILIYO BORA YASISITIZWA MASHULENI

Tarehe ya Kuwekwa: June 10th, 2025


Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi Joyce Sipira, akisisitiza umuhimu wa ulaji wa mazao lishe kwa wanafunzi kama njia ya kuboresha afya, kuongeza umakini darasani, na kuimarisha ufaulu wa kitaaluma.


Akizungumza leo katika mkutano na waandishi wa habari  Bi Joyce alisema kuwa kampeni hiyo inalenga kuhamasisha shule za sekondari kuanza kutumia mazao lishe yaliyothibitishwa kuwa na virutubishi muhimu kwa afya ya mwanafunzi. Alieleza kuwa tayari Halmashauri kwa kushirikiana na mdau wa lishe, HarvestPlus, imeanza utekelezaji wa mpango huo katika shule mbili za sekondari: Maposeni na Magagula.

“Tulipokea maelekezo kutoka kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambayo nayo ilipokea ugeni kutoka kwa mdau HarvestPlus wasambazaji waliothibitishwa wa mazao lishe. Kwa kuanzia, shule mbili zimechaguliwa kama sehemu ya majaribio ya mpango huu,” alisema Bi Joyce.


Aliendelea kufafanua kuwa lengo kuu la mpango huo ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata chakula chenye virutubishi vya kutosha ili waweze kuwa makini zaidi darasani, kupunguza utoro, kuongeza ushiriki wa darasani, na kuimarisha afya kwa ujumla.


Katika mkutano huo, Bi Joyce alitaja baadhi ya mazao lishe yanayopendekezwa kuwa ni mahindi ya njano lishe, viazi vitamu vya chungwa (viazi lishe), mihogo iliyoboreshwa, na maharagwe lishe yenye madini chuma kwa wingi. Alisema vyakula hivyo vina virutubishi kama vitamini A, madini ya chuma na zinki ambavyo husaidia kupambana na matatizo ya lishe duni kama vile udumavu, upungufu wa damu, uzito pungufu na utapiamlo.


“Kwa kushirikiana na mdau HarvestPlus, tuligawa kilo 200 za unga wa mahindi lishe katika shule hizo mbili  kila moja ikipokea kilo 100. Unga huo ulitumika kupika uji na ugali kwa wanafunzi. Tumeona mwitikio chanya na wanafunzi wameonyesha kufurahia sana aina hiyo ya chakula,” alieleza.


Bi Joyce alihitimisha mkutano kwa kutoa wito kwa serikali na wadau wa lishe kuongeza jitihada za kutoa mbegu bora, mbolea, na kuweka mikakati endelevu ya mpango wa utoaji wa chakula mashuleni ili kusaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, KARIBU RUVUMA UJIO WAKO NI MUHIMU KWA MASLAHI YA SONGEA DC

    July 27, 2025
  • MFUMO WA NeST UMEBORESHA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA MANUNUZI YA UMMA

    July 21, 2025
  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa