• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

KAYA masikini waanza kulipwa "kidigitali",walengwa walalamikia utaratibu huo

Tarehe ya Kuwekwa: January 14th, 2022

Mfuko wa kuhudumia kaya maskini nchini  katika Halmashauri ya wilaya ya songea Mkoani Ruvuma umeanza utaratibu wa kuwalipa fedha walengwa wa kaya maskini kwa njia ya kidigitali huku baadhi ya  walengwa wa mfuko huo wakilalamikia changangamoto ya ukosefu wa mawasiliano ya mtandao wa simu na baadhi yao kutojua kabisa matumizi ya simu.

Mratibu wa TASAF wa Halmashauri hiyo Hossana Ngunge amesema utaratibu huo umeanza kutumika mwezi Julai 2021 na kuendelea  hivyo walengwa wote wanatakiwa kujisajili kwenye mitandao ya  simu ambayo wataitumia kupokelea fedha zao.

Ngunge ametoa ushauri kwa makampuni ya simu kutumia fursa ya kwenda katika maeneo ambayo bado hayana mawasiliano ya simu na yenye mawasiliano yasiyokuwa na uhakika kuyafikia maeneo hayo ili walengwa wa kaya maskini  na wananchi wengine waweze kunufaika na huduma hizo.

Ameongeza kwakusema utaratibu wa kuwalipa kaya maskini kwa njia ya simu kutasaidia kuondoa changamoto ya gharama za zoezi la kuwafikishia walengwa fedha zao na baadhi ya walengwa kudhulumiwa na watu wasio waaminifu ambao waliokuwa wakiwatuma kuwachukulia faedha hizo.

Kwa upande wao baadhi ya walengwa wa kaya maskini wameulalamikia  utaratibu wa kupokea fedha kwa njia ya simu kwao umekuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na wao kutokuwa  na uelewa  juu ya matumizi sahihi ya simu hivyo kupelekea fedha zao kuporwa na wategemezi wao bila wao kutambua na kuomba wapatiwe fedha zao kwa njia ya tasilimu.

Halmashauri ya Wilaya ya Songea ina jumla ya kaya masikini 6,143 kati ya kaya hizo  3,731 ziliingizwa kwenye mpango tangu awamu ya kwanza kutoka Vijijiji 32  na awamu ya pili kaya 2,412 zimeingizwa kwenye mpango wa kupima matokeao ya kunusuru kaya masikini kwenye vijiji 24 na wataanza kulipwa baada ya kufanyiwa tathimini.

Imeandaliwa na kuandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari

Songea DC.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa