• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Kamati ya Uhamasishaji kutoka Or- TAMISEMI Yaridhishwa na Zoezi la Uandikishaji Halmashauri ya Wilaya ya Songea

Tarehe ya Kuwekwa: October 15th, 2024


Kamati ya uhamasishaji wa uandikishaji katika daftari la kudumu la kupiga kura kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ikiongozwa na Abdulrahman Hatibu, imefanya ziara ya kuhamasisha wananchi katika kata mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Songea. Ziara hiyo imelenga kutathmini mwenendo wa uandikishaji na kujionea hali ya mwamko wa wananchi katika kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.


Katika ziara hiyo, Hatibu alieleza kuridhishwa na mwitikio wa wananchi katika kujiandikisha akisema kwamba zoezi limeendelea kwa kasi nzuri. "Ikiwa tupo katikati ya siku za uandikishaji, tayari kata nyingi zimefanikiwa kufikia nusu au hata zaidi ya nusu ya malengo yao," alisema Hatibu huku akionyesha matumaini kuwa malengo yote yatatimia baada muda kuisha.


Hata hivyo, alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wananchi ambao bado hawajajiandikisha kuchukua hatua haraka kabla ya muda kuisha. “Tumeridhishwa na zoezi la uandikishaji, lakini nitoe wito kwa wale wote ambao hawajajiandikisha kujitokeza kwani muda bado upo, na ni haki yao ya msingi kama raia wa Tanzania,” alisisitiza Hatibu, akihimiza umuhimu wa kila raia kushiriki kwenye mchakato wa uchaguzi.


Ziara hiyo imekuwa ni sehemu ya kampeni kubwa inayosimamiwa na TAMISEMI kuhakikisha wananchi wanapata fursa ya kujiandikisha kwa wingi katika daftari la kudumu la wapiga kura. Kamati hiyo imekuwa ikiendesha mikutano na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiandikisha ili kuhakikisha sauti zao zinasikika katika chaguzi zijazo.


Kwa ujumla, uandikishaji umeonekana kupata mwitikio chanya kutoka kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, hali inayoashiria uelewa mzuri wa haki zao za kidemokrasia na umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi ujao.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa