• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Kamati ya Fedha, Uongozi, na Mipango Yaendelea na Ukaguzi wa Miradi ya Zahanati Kuboresha Huduma za Afya

Tarehe ya Kuwekwa: September 4th, 2024


Halmashauri ya Wilaya ya Songea, kupitia Kamati ya Fedha, Uongozi, na Mipango (KFUM) inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Mheshimiwa Menans Komba, imefanya ziara yenye lengo la kukagua na kusimamia miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha huduma za afya katika zahanati za vijijini. Miradi hii imedhaminiwa kupitia mpango wa Sustainable Rural Supply and Sanitation, ikilenga kuboresha miundombinu ya afya kwa wanawake na watoto.


Katika ziara ya leo, kamati imeweza kushuhudia mafanikio makubwa ya ujenzi na maboresho ya vyumba vya mama na mtoto, vyenye huduma muhimu kama vile chumba vya kujifungulia, maeneo ya kupumzikia, pamoja na miundombinu ya maji safi. Uboreshaji huu unaendana na jitihada za Halmashauri katika kuboresha huduma za afya kwa jamii, hasa kwa makundi nyeti kama vile wanawake wajawazito na watoto wachanga.


Zahanati zilizokaguliwa ni pamoja na Zahanati ya Kijiji cha Mpangula, Kata ya Matimila, Zahanati ya Kijiji cha Liweta, na Zahanati ya Kijiji cha Nakahuga, ambazo zote zimenufaika na kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya kisasa vya mama na mtoto, vyoo, na miundombinu ya maji safi.


Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Menans Komba, amesisitiza kuwa miradi hii ni sehemu ya jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuimarisha huduma za afya vijijini. Ameeleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa na kutoa pongezi kwa wadau wote waliohusika katika kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa weledi mkubwa. Pamoja na mafanikio yaliyopatikana, tathmini zaidi itaendelea kufanyika ili kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.


Halmashauri ya Wilaya ya Songea imeendelea kuonyesha dhamira ya dhati ya kuboresha huduma za afya na kuleta maendeleo endelevu kwa jamii.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa