• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

JENISTA MHAGAMA AMEWATAKA WANANCHI WA SONGEA KUFANYA KILIMO CHA KIBIASHARA

Tarehe ya Kuwekwa: July 9th, 2024


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho ameomba wananchi kuanza kujiandaa ili kulifanya zao la Mahindi kuwa zao la biashara kwa siku za usoni.

Waziri ametoa kauli hiyo katika ziara yake katika kata ya Matimila ambapo amefanya Mikutano miwili ya hadhara katika vijiji vya Kikunja na Mpingi vilivyopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma Leo tarehe 08/07/2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu ameendelea kutoa ruzuku ya mbolea, kazi kubwa kwetu wakulima ni kuongeza juhudi katika kilimo na uzalishaji wa mahindi.

Waziri Mhagama amesema, “Mwaka huu Mhe. Rais, ametutafutia masoko Nje ya Nchi, lengo letu ni kuhakikisha siku za karibuni tunafanya zao la mahindi kuwa zao la biashara ili liweze kusaidia wananchi kukuza uchumi na pato la familia.”

Aidha Waziri amewaomba wananchi kuendelea kuweka akiba ya chakula cha familia badala ya kuuza chakula chote ili nchi iendelee kuwa na akiba ya chakula.

Waziri ameelezea wananchi kuhusu fursa ya mikopo yenye masharti nafuu, ambapo amewaasa kutumia wasaa huo kufungua shughuli mbalimbali za uchumi, ikiwemo mashine za kusaga za umeme, na kujikita katika kuwekeza katika viwanda vidogo vidogo vya kuchoma chuma.

“Nishati ya umeme inatakiwa kuwasaidia wananchi kupata mapato na shunguli za kukuza kiuchumi,” alisema Waziri Mhagama

Awali Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Ndg. Mtela Mwapamba amewaambia wananchi kwamba watafanya mikutano ya ujirani mwema kati ya Mkuu wa Wilaya ya Songea na Wilaya ya Namtumbo na Kamati za ulinzi na Usalama ili kutatua migogoro ya Mipaka inayohusianisha wilaya hizo mbili.

Aidha Katibu Tawala amewaahidi wananchi wa kijiji cha Kikunja kwamba Serikali kupitia Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Songea , itawasaidia kuanzishwa kwa chama chao cha Ushirika katika Kijiji hicho ambacho hakina (AMCOS) Agricultural Marketing Cooperative Society.

“Kuanzishwa kwa AMCOS itasaidia Serikali kupata mapato hivyo ni jukumu la Watendaji wa Serikali kuhakikisha inasimamia mchakato na kanuni za uanzishwaji wake tangu mwanzoni mpaka ukamilikaji wake na kuhakikisha tunailea,“alisema Ndg. Mwapamba

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa