• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

IDADI YA WANAFUNZI WALIORIPOTI SHULENI YAONGEZEKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Tarehe ya Kuwekwa: February 7th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Kapenjama Ndile jana terehe 07/02/2024 alikutana na Wakuu wa Shule zote za Msingi na Sekondari wa Halmashauri ya Songea ili kupata Taarifa ya uandikishaji na uripoti wa wanafunzi wa  Darasa la Awali, Darasa la kwanza na Kidato cha kwanza 2024 .
Aidha Mkuu wa Wilaya alipongeza jitihada zinazofanywa na wakuu wa Shule ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji uliopelekea  kuongeza idadi ya wanafunzi wa darasa la Awali, Kidato cha kwanza na Darasa la kwanza ukilinganisha na hali ilivyokua katika kikao kazi cha tarehe 17/01/2024.

Mhe. Ndile ameyasema hayo kwenye kikao cha wakuu wa shule watendaji wa vijiji na kata na maafisa elimu wa kata kilichofanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari  Maposeni. Pamoja na wadau wengine wa Elimu, Mkuu wa Wilaya aliambatata na Katibu tawala wa Wilaya Mr. Mtela Mwampamba, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Mwl. Neema Maghembe pamoja na Maafisa Elimu Msingi na Sekondari

“Lengo la Halmashauri kwa mwaka 2024, ni kuhakikisha watoto wote walioandikishwa kuanza Elimu ya Awali 3946 na Darasa la kwanza 4123 wanaandikishwa kwa asilimia 100. Aidha kwa upande wa Sekondari, Halmashauri itahakikisha wanafunzi wote 2605 waliofaulu na kupangiwa shule za Kata wanaripoti kwa asilimia 100”

Uandikishaji kwa mwaka 2024 umeanza na unaendelea vizuri kwani hadi sasa jumla ya wanafunzi  wa Awali 4609 ambao ni sawa na asilimia 93% wameandikishwa shule na wanafunzi 4587 wa darasa la kwanza ambao ni sawa na asilimia 94% ya waliotarajiwa wameandikishwa.

Aidha jumla ya wanafunzi 4480  wa darasa la Awali na  ambao ni sawa na asilimia 97% na wanafunzi 4536 wa darasa la kwanza sawa na asilimia 99 ya walioandikishwa wameripoti Shulen na wanaendelea na masomo

Kwa upande wa shule za sekondari,jumla ya wanafunzi 2117 sawa na asilimia 81 wameripoti shuleni na wanaendelea na masomo huku juhudi zaidi zinaendelea kufanyika  ili kuhamasisha  wazazi/walezi kupeleka watoto shuleni. Sambamba na kuwafuata wanafunzi waliofaulu nyumba kwa nyumba ilikujiunga na shule

Katibu tawala wa Wilaya ya Songea, Mtela Mwampamba asisitiza mambo mawili:- wanafunzi wote wenye sifa na waliofaulu kuingia kidato cha kwanza, wafike mashuleni Wazazi na walezi wahakikishe wanawaepusha watoto ( wanafunzi) na ajira za mashambani, kwa kufanya hivyo ni kuhatarisha  usalama wao na kuwakosesha haki yao ya msingi ya kupata elimu.

Ikumbukwe kwamba, Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa Elimu bure kwanzia Awali, Msingi na Sekondari

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa