• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHURI YA WILAYA YA SONGEA KUJIANDAA KUPOKEA NEEMA YA UWEKEZAJI KIWANDA CHA SUKALI .

Tarehe ya Kuwekwa: January 9th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Songea Mhe Kapenjama Ndile amewataka wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea kukaa tayari kuupokea uwekezaji wa kiwanda kikubwa  cha sukari katika Kata ya  Lilyai Kijiji cha Magwamila.

Ameyasema hayo wakati akizungumza katika kikao na wataalamu wa ardhi wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea, wataalamu wa bodi ya sukari Tanzania na wawekezaji wenyewe kutoka Madwani Group kilichofanyika Leo 09.01.2024 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Songea. Ambapo Kapenjama Ndile ameeleza kwamba,

"Songea Sukari ni kiwanda kitakachojengwa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Kata ya Lilyai Kijiji cha Magwamila hivyo Leo tunafanya mapitio ya maombi ya wawekezaji ambapo wao wanatarajia kuweka zaidi ya Bilioni 500 katika kiwanda hicho, ambapo kiwanda  kitazalisha Tani zaidi ya laki moja kwa mwaka, pia kitaweza kuzalisha umeme ambao utaweza kuuzwa kwenye grid ya Taifa, pia kitazalisha mafuta aina ya ethane hivyo kuwepo kwa kiwanda hicho kitaleta manufaa makubwa sana katika Halmashuri yetu hivyo nitoe wito kwa wananchi wa Wilaya ya Songea hususani Songea vijijini kupokea mradi huu kwa mikono miwili".

"Nae Mchumi mwandamizi wa Bodi ya Sukari Tanzania Joshua Mhando amesema " kwa ujimla Bodi ya Sukari Tanzania inashukuru sana kwa mchakato mzima unaondelea hapa Halmashuri ya Wilaya ya Songea kwani kwetu sisi tunapendezwa sana na uwekezaji wa uzalishaji wa sukari katika nchi yetu pia tunawashukuru sana wawekezaji kwa kuweka Nia ya kuwekeza katika Wilaya hii, hivyo napenda kuishukuru sana Serikali chini Raisi wetu Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji nasi tunamuahidi kutoa ushirikiano ili kuleta maendeleo katika Taifa letu"

Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Ndg Makisio Chengula amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Songea kwaajili ya kikao hicho cha mapitio hayo ya maombi ya uwekezaji katika Halmashuri ya Wilaya ya Songea kwani kupitia wawekezaji hao Halmashauri itaweza kuingiza fedha nyingi kama mapato, pia amemshukuru Mhe Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika nchi yetu hususani katika Halmashuri  ya Wilaya ya Songea.

Pia mjumbe wa Madwani Group ( mwekezaji) Kapil Dave amemshukuru kwa mapokezi mazuri waliyoyapata na kuwezesha kikao hicho kufanywa kwa amani, pia ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuweka utaratibu mzuri wa uwekezaji katika nchi hii na amesema iwapo watapewa nafasi ya kuwekeza katika eneo hilo la Magwamila basi ameahidi kufanya uzalishaji wenye tija na wenye kuleta maendeleo chanya katika jamii na nchi kwa ujumla.

Eneo la uwekezaji linatarajiwa kuwa na ukubwa wa hekta elfu 30 ambapo hekta elfu 22 zitakuwa kwaajili ya Kilimo cha miwa na hekta elfu 8 kwaajili ya huduma nyingine ikiwa ni pamoja na ufungaji wa mitambo (kiwanda), barabara za ndani, maghara, makazi ya watumishi ( vibarua ) ujenzi wa huduma za kijamii ikiwemo shule pamoja vituo vya afya. Sambamba na hilo wananchi watapewa hekta elfu 14 kwaajili ya kilimo cha miwa ambayo wataiuza katika kiwanda hicho ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa