• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HAKUNA mwanafunzi atakateye baki nyumbani 2021

Tarehe ya Kuwekwa: January 13th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Chirstina Mndeme amesema Mkoa umejipanga vizuri katika kuhakikisha Watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza Januari  2021 wanaanza kidato cha kwanza bila vikwazo vyovyote.

Mndeme ametoa kauli hiyo kwenye kikao cha kamati ya ushauri cha Mkoa kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Mndeme amesema Mkoa wa Ruvuma umejipanga vizuri katika swala zima kuhakikisha watoto wote walio chaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanaanza masomo bila kikwazo kwasababu miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia ipo na inakidhi mahitaji.

“Tunahitaji jitihada za pamoja kuongeza ufaulu”,amesema Mndeme.

Akiongelea kuhusu ufaulu Mndeme amesema mwaka 2020 ufaulu ni asilimia78.52 na umeshuka  kwa asilimia 5.12 ukilinganisha na mwaka 2019 ufaulu ulikuwa asilimia 83.70  kwa wanafunzi wa darasa la saba hivyo zinahitajika jitihada za pamoja ili kuongeza ufalu  katika Halmashauri zote.

Ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kushika nafasi ya kwanza Kimkoa kwa kufaulisha kwa asilimia 85.51 huku akiitaka Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuongeza jitahada za kufaulisha kwani imekuwa ya mwisho, na imefaulisha kwa asilimia 66.8 kinyume na lengo la Mkoa la kufaulisha kwa asilimia 90.

Mndeme amewapongeza walimu wa shule za sekondari kwa kufaulisha wanafunzi wa kidato cha sita kwa asilimia 98.8 mwaka 2020.

Ametoa wito kwa kamati ya ushauri ya Mkoa kushirikiana kwa pamoja kujenga shule ya wasichana katika Halmashauri ya Madaba ambayo itachukua wanafunzi kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma  kwa lengo la kuwanusuru watoto wa kike na vikwanzo ambavyo vinakwamisha jitihada zao za kusonga mbelea na masomo.

Baadhi ya wazazi na walezi wamezidi kuipongeza serikali kwa mpango wa Elimu bure,mpango ambao umewasaidia kuwapeleka Watoto wao shule kwa wakati na Watoto wote wanaostahili kwenda shule na kuto wapangia majukumu ambayo si yao kama vile kuchunga mifugo na kuchuuza bidhaa.

Imeandikwa na

Jacquelen Clavery-Kitengo cha Habari

Songea DC.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa