• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Chanjo ya saratani yamlango wa kizazi

Tarehe ya Kuwekwa: April 25th, 2018

CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI.

Wananchi wametakiwa kutambua chanjo dhidi ya ugonjwa wa saratani y mlango wa kizazi nichanjo salama na haina madhara yoyote kwa watoto wakike

Hayo  yamesemwa na wataalam mbalimbali wa afya katika  zoezi la uzinduzi wachanjo ya saratani ya mlango wa kizazi uliofanyika katika shule ya Sekondari Maposeni Mji mdogo wa Peramiho.

Wataalam hao wamesema chanjo hiyo ni salama na haina madhara kwakuwa imethibitishwa na shirika la Afya duniani na Mamlaka ya chakula na dawa nchini hivyo wananchi waondoe hofu kwa watoto wao watakao patiwa chanjo hiyo.

Mganga mkuu wa wilaya ya Songea Dr Yesaya Mwasubira amesema chanjo hiyo imefanyiwa majaribio katika Mkoa wa Kilimanjaro na kutoa mafanikio makubwa.

Amesema chanjo zote zinazotolewa dhidi ya magonjwa zina faida nyingi kama kuepukana na magonjwa,kupunguza vifo katika jamii na kujengaTaifa la watu wenye afya bora .

Amesema walengwa wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi ni wasichana wato wenye umri wa  miaka kumi na nne (14) mwaka 2018 na mwaka 2019 wataanza kuchanja wasichana wenye umri wamiaka 9,wameanza kuchanja kundi hilo kwasababu kundi ambalo linakaribia kujihusisha na mapenzi. chanjo hiyo hutolewa bure na endelevu kama chanjo nyingine zinazotolewa

Adha Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya wilaya ya Songea Bw Simon Bulengenije ametoa wito kwa wananchi kuwa waruhusu watoto wao kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi ili waweze kuepukana na maambukizi ya virusi vinavyo sababisha ugonjwa huo ambao hauna tiba dhidi yakujikinga tu.

Amewataka wahudumu wanao husika na zoezi la utoaji wa chanjo kuwafikia walengwa wote hata wale wasio kuwa mashuleni katikaHalmashauri na kuendelea kutoa elimu kuhusu madhara makubwa yatokanayo na ugonjwa wa saratani kwa familia,jamii,na Taifa.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Mh Pololeti Mgema ametoa onyo kwa mtu yeyote atakaye thubutu kuhujumu zoezi la uchanjaji wa chanjo mpya ya saratani ya mlango wa kizazi atachukuliwa hatua za kisheria bila kujali wadhifa wake na kuendelea kuunga mkonojitihada za serikali katika kuhamasisha maendeleo.   

Ugonjwa wa saratani  ya mlango wa kizazi ni ugonjwa unaongoza kusababisha vifo kwa wanawake wengi kwa asilimia 50 ukilinganisha na magonjwa mengine. Dalili zake kutokwa damu bila mpangilio au baada ya kujamiina,maumivu ya mgongo,miguu,na kiuno,kuchoka,kupungua uzito,kukosa hamu ya chakula na kutokwa uchafu kwenye uke wa majimaji,uliopauka wa rangi ya kahawia au wenye damu.

Na husababishwa na kuanza kujamiiana katika umri mdogo,kuwa nawapenzi wengi, ndoa za mitala,kuzaa watoto wengi nauvutaji wa sigara.

Halmashauri ya wilaya ya Songea inatarajia kutoa chanjo kwa mabinti zaidi ya 2000 .

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa