• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

ARDHI Ruvuma yavuka lengo la ukusanyaji maduhuli ya serikali

Tarehe ya Kuwekwa: March 1st, 2021

KAIMU Kamishina wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Ruvuma Ildeforce Ndemela amesema Idara ya ardhi mkoani Ruvuma imekusanya maduhuli ya serikali kwa asilimia 108.

Akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelina Mabula,Kaimu Kamishina wa ardhi amesema kiasi hicho cha fedha kimekusanywa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.

Ndelema amesema serikali iliupangia Mkoa wa Ruvuma kukusanya maduhuli ya serikali ya shilingi 990,000 hadi kufikia Juni 30,2020 na kwamba Idara ilifanikiwa kukusanya shilingi bilioni 1,076,957,355.22 sawa na asilimia 108.

“Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 Idara ya Ardhi Mkoa wa Ruvuma imepangiwa lengo la kukusanya kiasi cha bilioni 4.6, hadi kufikia Februari Mkoa umekusanya shilingi milioni 740 sawa na asilimia 16,mikakati ya kuongeza makusanyo ya kodi ikiwemo ikiwemo kuandaa na kusambaza ankra za umiliki na Hati za madai ya kodi’’,alisema Ndemela.

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma katika kipindi mwaka 2020/2021 umepangiwa lengo la kupima viwanja 16,550 na mashamba 104 ambapo hadi kufikia Februari 22,2021,viwanja 4,873 na mashamba matano yamepimwa katika maeneo ya mijini na vijiji kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Amesema Idara hiyo imepokea jumla ya michoro ya mipango miji 41  yenye jumla  ya viwanja 18,581 vya matumizi mbalimbali na kwamba zoezi la kurasimisha makazi holela linaendelea katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelina Mabula akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo amesema ukusanya maduhuri ya serikali kitaifa katika Wizara yake  imefikia asilimia 30 na Mkoa wa Ruvuma umefikia asilimia 16.

Kutokana na hali hiyo Naibu Waziri Mabula ameziagiza Halmashauri zote nchini kuongeza juhudi za ukusanyaji maduhuli ya serikali ili kufikia malengo waliojiwekea ikiwemo kukusanya madeni kwa kuzingatia sheria.

“Sheria ipo wazi,kifungu cha 50 kifungu kidogo cha kwanza cha sheria ya ardhi namba nne kinampa siku 14 tu mdaiwa anapokuwa amepewa Ilani,ndani ya siku 14 asipoweza kulipa,tunampeleka kwenye Baraza, kinachofuata ni yeye kulipa deni’’,alisisitiza.

Amesema ikishatolewa oda ya kutakiwa kulipa anatakiwa kulipa au kukamata mali zake na kuuzwa ili fedha ipatikane ambapo amewataka watendaji wa Ardhi waache kugeuza ukusanyaji maduhuli kuwa kufanyika kisiasa.

Dkt.Mabula amewaagiza maafisa ardhi kuongeza kasi ya kupima viwanja na mashamba na kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa maafisa ardhi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ikiwemo upangaji, upimaji, umilikishaji.uthamini,usajili wa hati,utatuzi wa migogoro ya ardhi na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali.

Imeandikwa na jacquelen clavery

Afisa Habari songeadc

Machi,Mosi,2021

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • WASIRA ATIA NENO UKAMILISHAJI WA MIRADI SONGEA DC, AMPONGEZA DKT. SAMIA

    June 12, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA SONGEA AWAPONGEZA WATENDAJI WA HALMASHAURI KWA KUSIMAMIA VIZURI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE BORA

    June 11, 2025
  • MATUMIZI YA LISHE ILIYO BORA YASISITIZWA MASHULENI

    June 10, 2025
  • KITUO CHA AFYA MATIMILA CHAKABIDHIWA GALI LA WAGONJWA.

    June 06, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa