• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WILAYA ya Songea imeingia mkataba wa kukusanya shilingi milioni 950 na Kampuni ya WFC LTD

Tarehe ya Kuwekwa: March 10th, 2021

 Halmashauri ya wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imeingia mkataba na kampuni ya West Food Comp LTD ya kutoka Makambako Mkoani Njombe kwa ajili ya kukusanya ushuru wa mazao.

Makubaliano ya mkataba huo yamefanyika leo katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji  kwa kuwekeana saini baina ya Mkurugenzi wa Kampuni na Uongozi wa  Halmashauri.

Akisaini mkataba huo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Tanu Kameka ametoa wito kwa Kampuni kufanya kazi waliyoomba kwa ufanisi kwasababu Serikali inategemea mapato kwa ajili ya kutekeleza majukumu  yake.

 Mweka hazina wa Halmashauri hiyo Rajabu Lingoni amesema katika kuboresha ukusanyaji wa mapato vikao vya kisheria vilikubaliana kumpata mzabuni atakayefanya kazi ya ukusanyaji wa ushuru wa mazao baladala ya kuendelea kuwatumia mawakala.

 “Utaratibu wa kutumia zabuni katika kukusanya ushuru wa mazao utadhibiti mapato” Amesema lingoni.

Amesema maamuzi ya kumtumia mzabuni ni jambo nzuri  litakalo saidia  kudhibiti mapato ya Halmashauri,maamuzi hayo yamefikia baada ya kubaini unaudanganyi mkubwa katika ukusanyaji wa ushuru,unaofanywa na baadhi wa Tendaji wa Kata kupitia mawakala wao kitendo ambacho kilikuwa kinakwamisha jitihada za Halmashauri katika kutekeleza majukumu yake.

Lingoni amesema jumla ya vizuio 15 vimeanishwa na vimekabidhiwa kwa mzabuni ambavyo vitatumika katika kukusanya ushuru wa mazao kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Machi 2021hadi Machi 2022.

Lingoni amesema mzabuni anatakiwa kukusanya ushuru kwa kuzingatia taratibu,kanuni na sheria za ukusanyaji wa mapato zilizowekwa na Serikali na Halmashauri pasipo kumbughuzi mtu yeyote na Ofisi ya Mkurugenzi itafanya shughuli ya usimamizi na ufuatiliaji katika zoezi hilo.

Kwa upande wake mhasibu wa mapato wa Halmashauri hiyo Noel Chengula amepongeza utaratibu wa kutoa zabuni katika kazi ya ukusanyaji ushuru ni kitendo kinachoonekana kitaongeza ufanisi na kuondoa usumbufu na gharama za kuwalipa mawakala ambao awali walikabidhiwa jukumu hilo.

Chengula amesema sambamba na kuongeza ufanisi jambo hilo litasaidi kupunguza changamoto ya madeni kwa baadhi ya Watendaji wa Kata na  Vijiji na mawakala,gharama za ufuatiliaji,na fedha kufikishwa bank kwa wakati

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni hiyo Godwin Chengula  amehaidi kufanyakazi  kwa ufanisi kwa sababu ni mzoefu katika kazi ya ukusanyaji ushuru ,na anafanyakazi hiyo katika maeneo ya Wilaya ya Ulanga ,Ifakara ,Makambako na Manispaa ya Songea

Imetaarishwa na kuandikwa na,

Jacquelen Clavery ,

Afisa Habari 

Songeadc.

 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, KARIBU RUVUMA UJIO WAKO NI MUHIMU KWA MASLAHI YA SONGEA DC

    July 27, 2025
  • MFUMO WA NeST UMEBORESHA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA MANUNUZI YA UMMA

    July 21, 2025
  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa