• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZIRI MKUU afungua kikao kazi cha Maafisa habari Serikalini Dar es salaam.

Tarehe ya Kuwekwa: March 27th, 2023


WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema Maafisa Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali wanao wajibu wa kuhakikisha wanatoa taarifa za jinsi serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya kipindi cha miaka miwili imefanya.


Mhe. Majaliwa ameyasema hayo wakati akifungua Kikao Kazi cha 18 cha Maafisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Machi 27, 2023


“Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini, mnao wajibu wa kuhakikisha mnatoa taarifa za jinsi serikali ilivyotatua shida hizo za wananchi kwani kwa kutofanya hivyo wapo watu wengine wataendelea kufanya upotoshaji wakati sisi wanahabari tunajua kuwa huo ni upotoshaji.”” Alifafanua.


Alisema jukumu la kuisemea serikali ni moja ya sehemu ya mawasiliano ya nje ya serikali kwahivyo wanapaswa kuzingatia.


Alisema sambamba na hilo, aliwataka wanahabari wote wa serikali na binafsi wahakikishe wananchi wanapata elimu na  taarifa sahihi kuhusu faida na umuhimu wa miradi na mipango au shughuli zinazotelekezwa na serikali ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa sahihi kwa urahisi  zaidi na kwa wakati.


Aidha aliwataka wazingatie suala la uhuru wa kupata na kutoa habari unaoendelea kutekelezwa kwa mujibu wa sheria, Taratibu na kanuni na wadau wote kila mmoja atimize wajibu wake.


Aliwataka kuimarisha matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuongeza upatikanaji wa habari kwenye maeneo yenu.“Kila mmoja kutoka mahali alipo, tunazo taasisi za mitandao ya kijamii ambazo zinafanya kazi pamoja na serikali, endeleeni kuwashirikisha katika kutoa taarifa za kazi na shughuli za serikali.” Alisisitiza.


Pia aliwataka kushiriki kikamilifu kuitangaza vema Tanzania ndani na nje ya nchi hususan sula la amani na utulivu, fursa za biashara na uwekezaji, historia ya nchi na kuweka msisitizo katika kufuata maadili na mila za nchi na kutangaza mali kale na vivutio


Aidha aliwataka kuweka mbele uzalendo, uadilifu, uhuru na maslahi ya nchi ili kulijenga taifa na aliwakumbusha kuongeza ubunifu wa kusukuma ajenda za serikali kwa umma.


Hali kadhalika aliwataka kujiendeleza ili kuendana na asi ya mabadiliko ya kiteknlojia.


Akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alisema Kikao hicho ambacho kimewaleta pamoja Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali kutoka Bara na Visiwani  ni muhimu kwa ustawi na mchango wa kada hii katika utekelezaji wa shughuli za kila siku za serikali.


“Kikao hichi kitatumika pamoja na mambo mengine kutathimini mchango wetu katika kusukuma ajenda mbalimbali za serikali na namna ya kuboresha mchango huo.” Alifafanua Mhe. Nnauye.


Katika hatua nyingine TAGCO kimempa tuzo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua na kuthamini mchango wake katika kuimarisha sekta ya habari, demokrasia, uwazi, uhuru wa kutoa maoni na kupata taarifa nchini.


Tuzo hiyo imepokelewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais.


Akikabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya TAGCO, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye alisema,  “Sisi maafisa habari serikalini, tumemwelewa, tunamwamini na tunamuunga mkono kwa dhati, Anaishi anayoyasema na anayatenda kwa ustadi mkubwa.” Alisema Mhe. Nape


Kauli mbiu ya Mwaka huu ni "Mawasiliano ya Kimkakati Injini ya Maendeleo".

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa