• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZIRI MKUU AAGIZA UHIFADHI WA HISTORIA WA KIUTAMADUNI

Tarehe ya Kuwekwa: February 27th, 2021

Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kassim majaliwa, ameziagiza mamlaka za mikoa na  serikali za mitaa kuhakikisha wanatenga bajeti,  kwa ajili ya kuibua,kutangaza na  kuhifadhi maeneo yote ya kihistoria.

 Maagizo hayo,yametolewa na Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Inocent Bashungwa kwa niaba ya waziri Mkuu, wakati akifunga Tamasha la kumbukizi la Vita vya majimaji na Utalii wa kiutamaduni, lililofanyika leo katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya majimaji Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma .

Waziri Mkuu  Majaliwa ameziagiza mamlaka za Mikoa na Serikali za mitaa  kutenga bajeti ,kwa ajili ya kuhakikisha maeneo yote ya kihistoria ya kiutamaduni yanatambuliwa na yanahifadhiwa kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho.

Ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo  kuendelea kuadhimisha kumbukumbu ya maadhimisho ya Mashujaa, kila mwaka ili kuhifadhi Historia ya nchi  na Ukombozi wa kusini mwa Bara la Afrika.

Ameongeza Wizara zote mbili zihamasishe jamii na kuelimisha kuwa, wanayofursa ya kumiliki maeneo ya Malikale na kuanzisha makumbusho kama sera ya malikale ya mwaka 2008 inavyofafanua.

“Mashujaa babu zetu wamepigana kwa ajili ya Taifa kilichobaki ni kwetu Vijana kutimiza wajibu, kupitia Vita vya majimaji ambavyo wazee wetu walipigania Uhuru, kwa kutumia mbinu mbalimbali, walipanda mbegu ya kizalendo,  vinatukumbusha ni kitendo cha  kizalendo kwa kuipenda Nchi yetu kwa kushirikiana, kushikamana wakaweza kuikomboa Tanzania” amesema Majaliwa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Cosmas Nshenyi amesisitiza Suala la Uzalendo kwa kuandaa taifa la kizalendo, ambalo litakuwa na jukumu la kusimamia na kuhifadhi historia ya Nchi na Utamaduni, wa Mtanzania kwa kuijali na Kuipenda Tanzania.

Naye Chifu wa kabila la wangoni Ema Nkosi wa Mamkos Emanueli Zulu Gama ameiomba Serikali kufanya mchakato wa kuipandisha hadhi, Makumbusho ya Taifa ya Majimaji kuwa makumbusho ya kwanza kusini mwa bara la Afrika, kwa kuwa makumbusho haya ya majimaji yamekuwa yanatoa fursa ya kushikiana na  Nchi nyingine za kusini mwa Bara la Afrika katika kufanikisha Tamasha la Kiutamaduni.

Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho Taifa Dr Noel Lwoga, amesema Makumbusho ni Taasisi ya Kielimu ambayo ina jukumu la kukusanya, kutafiti na kuhifadhi na kuelimisha jamii kuhusu urithi wa Taifa letu, hivyo linawajibu Mkubwa katika kufundisha na kuelimisha jamii kuhusu Historia ya Tanzania kwa Vitendo kupitia Tamasha la Kiutamaduni, na kukuza Utalii wa ndani wa kiutamaduni.

Aidha Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mali asili na Utalii christowaja Ntandu, amesema Wizara inamikakati ya kutangaza maeneo muhimu ya Kihistoria ya Viongozi wetu wa jadi, ya wapigania Uhuru na yale yenye historia ya Nyerere katika Mkoa wa Ruvuma na mikoa mingine Tanzania. Lengo ni kuyahifadhi na kuyaendeleza kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Utalii.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa