• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAZIRI MHAGAMA AAGIZA KUJENGWA STENDI YENYE UBORA KIJIJI CHA LUNDUSI

Tarehe ya Kuwekwa: September 17th, 2023


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amezitaka Idara zinazohusika na ujenzi katika Halmashauri kuhakikisha zinajenga stendi ya mabasi  yenye ubora unaoendana na thamani ya fedha zilizotolewa ili kujenga Stendi  hiyo  katika Kijiji cha Lundusi, Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Mhe. Jenista ametoa maagizo hayo wakati akizindua mradi wa ujenzi wa Stendi ya kisasa ya magari katika kijiji hicho unaotekelezwa na Ofisi ya Rais kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) utakaogharimu  shilingi Milioni 482 ukitarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi sita tangu kuanza kwa mradi.

Amesema  katika awamu  ya kipindi cha pili cha utekelezaji, TASAF imejikita  katika masuala ya kuwezesha Kaya kutumia fursa za kukuza Uchumi na kuongeza kipato kwa kaya zenye walengwa pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma za Afya, Elimu na Maji Safi na Salama pamoja na miundo mbinu  ya kukuza uchumi ngazi ya jamii.

“Wananchi wanasubiri Stendi bora ya kisasa na siyo stendi mbovu,idara zinazohusika na ujenzi kwenye Halmashauri sasa kumekucha na hatutarajii eneo la manunuzi ya ujenzi yakawa ni kichaka cha upotevu wa fedha kutoka Ofisi ya Rais kupitia Mfuko wa TASAF hivyo matumizi sahihi ya fedha yajidhihirishwe katika mradi huu,” Amesema Mhe. Jenista.

Aidha  Mhe. Jenista  ametoa wito kwa wataalam kutekeleza  majukumu yao kama inavyotakiwa hasa maafisa wa Idara ya Ujenzi, Manunuzi na Fedha ili kuepuka kusuasua kwa mradi huo pamoja na kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji katika ngazi zote kuanzia hatua ya awali hadi hatua ya mwisho ya ukamilishaji wa mradi.

 “TASAF ni chombo cha Serikali ambacho kinasaidiana na vyombo vingine kusaidia jitihada za kuondoa kero ya umaskini, upatikanaji wa maji safi na salama, elimu na afya ili kujenga Jamii iliyo bora, ambayo sisi sote ni mashahidi. TASAF imeleta mafanikio makubwa katika Nchi yetu kama ilivyoainishwa katika Mpango wa pili wa Taifa wa Maendeleo wa 2020/2025 kwa kutumia dhana ya ushirikishwaji wa Jamii,”Amebainisha Waziri huyo.

Akitoa  taarifa ya  Shughuli za TASAF katika Halmashauri ya  Wilaya ya  Songea  Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Neema Maghembe amesema kukamilika kwa ujenzi wa Stendi hiyo ya mabasi utarahisisha usafiri kwa wananchi watakaofika katika Halmashauri hiyo kupata huduma.

“Faida nyingine ni Mazingira bora kwa wafanyabiashara eneo la stendi, kuimarisha ulinzi na usalama katika eneo la stendi kwa wasafiri na wafanyabiashara , kuongezeka kwa pato la Halmashauri , kuongeza fursa  ya ajira kwa vijana  na wananchi pamoja na huduma ya usafiri kwa wanaosafiri kutoka nje na ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea,” Ameeleza Mkurugenzi huyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Bw.  Shedrack Mziray ameeleza kuwa Mfuko huo umekuwa ukitekeleza miradi ya maendeleo nchini kwa lengo la kukwamua Kaya masikini na hatimaye waweze kubuni na kuanzisha miradi yao binafsi ili kumudu gharama za maisha.

“Tunafanya utekelezaji katika maeneo manne Kitaifa tunafanya Uhawilishaji  wa fedha ambapo mpaka sasa tumehawilisha  shilingi Bilioni 919.6 tangu kuanza kwa  Awamu ya kipindi cha Pili mwaka 2020  na kufikia kaya zaidi ya Milioni 1.3. Pia tumefanya miradi ya ajira za muda karibu miradi 14,236 yenye thamani ya Bilioni 169 na kutoa ajira kwa Kaya zaidi ya 660,000 pamoja na miradi ya kukuza uchumi wa kaya,” Amesema  Bw. Mziray.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini Mhe. Menas Komba ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha kuhakikisha miradi mikubwa ya maendeleo inatekelezwa huku akiipongeza TASAF kwa kuanzisha mradi wa ujenzi wa Stendi ya Mabasi katika Kijiji cha Lundusi ambapo kukamilika kwake kutainua vipato vya wananchi na Taifa kwa ujumla.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa