• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Waziri Bashe Afanya Ziara Halmashauri ya Songea na Kukagua Vituo vya Ununuzi wa Mahindi,

Tarehe ya Kuwekwa: September 18th, 2024


Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Hussein Bashe, amefanya ziara ya kukagua vituo vya ununuzi wa mahindi katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, akiridhishwa na utaratibu uliowekwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) wa kununua mahindi bora.


Mhe  Hussein Bashe, ameendelea na jitihada zake za kuboresha sekta ya kilimo nchini kwa kufanya ziara ya ukaguzi katika vituo viwili vya ununuzi wa mahindi, Kizuka na Mgazini. Ziara hiyo imelenga kukagua utaratibu wa ununuzi wa mahindi katika vituo hivyo, ambapo aliridhishwa na hatua zinazochukuliwa na NFRA za kuhakikisha ununuzi wa mahindi yaliyochaguliwa kwa umakini.


Waziri Bashe, akizungumza na wakulima, aliahidi kuwa serikali itaongeza maghala ya kuhifadhia mazao ili kupunguza changamoto ya uhaba wa nafasi ya kuhifadhi mazao baada ya kuvuna. Aidha, alieleza mpango wa serikali wa kuboresha miundombinu ya usafiri, hususan barabara zinazoelekea vituo vya kuuza mazao, jambo ambalo litasaidia kupunguza gharama za usafirishaji kwa wakulima.

Katika hatua nyingine, Waziri Bashe alitoa ahadi ya kuweka mashine za kisasa za kuchambua mahindi katika msimu ujao wa kilimo. Alieleza kuwa mashine hizo zitapunguza muda wa kuchambua mahindi, tofauti na sasa ambapo wakulima wanatumia machekeche yanayochambua gunia moja kwa siku. Alisema, "Lengo ni kuhakikisha kwamba wakulima wanatumia muda mfupi kufanya kazi, hivyo mashine hizi zitasaidia sana katika kuboresha uzalishaji."


Waziri Bashe pia alizungumzia changamoto ya mbegu feki, akiahidi kuwa msimu ujao wakulima hawatouziwa mbegu zisizo na ubora. Alifafanua kuwa serikali itaimarisha udhibiti wa mbegu zinazouzwa madukani kwa kuweka mfumo wa kidijitali utakaowezesha wakulima kuhakiki ubora wa mbegu kabla ya kununua. "Tumechunguza na kugundua kuwa moja ya sababu za mahindi machafu ni kutokana na mbegu feki. Kwa hiyo, tutahakikisha mfuko wa mbegu unakuwa na 'barcode' ambapo mkulima ataweza kuingiza namba kwenye simu na kupata taarifa ikiwa mbegu ni feki au halali," aliongeza Waziri.


Wananchi wa Kizuka na Kilagano walimshukuru sana Waziri Bashe kwa kuwatembelea na kujionea changamoto wanazokabiliana nazo. Walitoa wito kwa serikali kuzifanyia kazi changamoto hizo ili kuboresha uzalishaji na kuleta tija kwa wakulima wa maeneo hayo.  


Ziara ya Waziri Bashe ni sehemu ya juhudi za serikali kuboresha sekta ya kilimo, ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi wa taifa, na kuhakikisha kuwa wakulima wanapata mazingira bora ya kuzalisha mazao kwa tija zaidi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa