• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WATAALAMU washauriwa kushirikiana katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko

Tarehe ya Kuwekwa: October 6th, 2020

MTAALAMU wa Epidemiolojia na Udhibiti wa  Magonjwa wa Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto Dr.Azma Simba, ametoa rai kwa wataalam kuungana na kushirikiana  ili  kukabiliana na magonjwa ya milipuko na kuimarisha usalama wa afya duniani.

Dr.Simba ametoa rai hiyo wakati anawasilisha mada ya agenda ya kukabiliana na matukio muhimu ya kiafya ya kimataifa, kwenye mafunzo ya utayari wa kukabiliana na magonjwa mlipuko kwa timu za dharura kwa wataalam kutoka mikoa ya Ruvuma na Mtwara.

Akizungumza katika mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Tiffany mjini Mtwara, Dr.Simba amesema dunia imeathirika zaidi na magonjwa ya milipuko yakiwemo ebola na COVID 19 na kwamba mwaka 2014 Agenda ya Afya Duniani ilianzishwa kwa lengo la kuhakikisha Dunia inakuwa salama kutokana na milipuko ya magonjwa hayo.

“Nchi nyingi duniani zimeweka jitihada kubwa katika kujilinda na magonjwa ya mlipuko,hata hivyo ni vema watalaam kufanya kazi kwa ushirikiano ili pawepo na usalama wa afya duniani’’,alisema.

Mtaalam huyo wa kudhibiti magonjwa amesema, kupitia agenda ya afya duniani,imetolewa miongozo na kanuni za kimataifa zinazoongoza kukabiliana na magonjwa ya milipuko.

Ameyataja madhumuni ya Agenda ya afya ya dunia kuwa ni  kuwepo kwa mifumo ya afya ambayo imejikita kuzuia,kutambua mapema na kukabiliana na ugonjwa unapotokea na kwamba milipuko mingi ya magonjwa inayotokea inaweza kuzuilika kwa njia ya chanjo.

Hata hivyo ametoa rai kwa  timu za dharura za kukabili magonjwa ya mlipuko katika ngazi za Halmashauri na Mkoa  kufanya ufuatiliaji wa magonjwa kwa wakati na kutoa taarifa mapema katika ngazi husika.

Kwa upande wake Daktari wa mifugo  Dr.Moses Ole Neselle kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani(FAO) akitoa mada kwenye mafunzo hayo,ameyataja magonjwa sita ya kipambele ambayo yanaambukiza kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kuwa ni Kichaa cha mbwa  ambacho kinatarajiwa kutokemezwa mwaka 2030.

Ameyataja magonjwa mengine kuwa ni homa ya bonde la ufa,kutupa mimba kwa wanyama,mafua ya ndege,kimeta na ugonjwa wa ebola na amesisitiza kuwa magonjwa hayatambui mipaka ya nchi hivyo ni vema wataalam wote kushirikiana kukabiliana na magonjwa hayo.

Amesema asilimia 50 ya magonjwa yote yanaambukizwa kupitia virusi na kwamba asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na wanyamapori hivyo ameshauri kuwepo mpango mkakati wa kukabiliana na magonjwa hayo.

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Profesa Rudovick Kazwala imesisitiza kuwa katika kutokomeza magonjwa ya mlipuko ni lazima wataalamu wafanye kazi kwa kushirikiana ili kutoa matokeo chanya.

Imeandikwa na Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea DC

Mtwara

Oktoba 6,2020

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa