• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Wataalamu wa Kilimo Songea DC Wapongeza Wakulima wa Parachichi Peramiho

Tarehe ya Kuwekwa: October 1st, 2025


Leo Oktoba 1, 2025 Timu ya wataalamu kutoka Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ikiongozwa na Ndugu Godson Msalilwa, imeendelea na ziara ya kukagua na kutoa elimu kwa wakulima wa zao la parachichi katika Kata ya Peramiho.


Katika ziara hiyo, Ndugu Msalilwa aliwapongeza wakulima kwa kujitolea na kuwekeza katika zao hilo, akibainisha kuwa parachichi ni moja ya mazao ya kimkakati ambayo Halmashauri imepanga kuyawekea mkazo kutokana na faida zake za kiuchumi na uendelevu. Aliongeza kuwa parachichi ni zao la kudumu linaloweza kuwainua wakulima kiuchumi ukilinganisha na mahindi ambayo kwa muda mrefu yamekuwa tegemeo kubwa la wakulima wengi.


"Tunawapongeza kwa kuwa wakulima wa mfano mliothubutu kuwekeza kwenye parachichi. Zao hili lina tija kubwa na litasaidia kuinua kipato cha kaya zenu endapo mkizingatia kanuni bora za kilimo," alisema Msalilwa.


Aidha, aliwaelekeza wakulima hao kuzingatia mambo matatu muhimu ili kupata mazao bora ya parachichi, ambayo ni: usafi wa shamba, matumizi ya mboji au samadi, pamoja na kuhakikisha uwepo wa maji ya kutosha kipindi cha masika na kiangazi.

Kwa upande wake, Afisa Kilimo wa Halmashauri hiyo, Frank Sungau, aliwasisitiza wakulima kutumia dawa za kuua wadudu waharibifu na mbolea kwa wakati unaotakiwa, ili kuongeza tija na ubora wa mazao yao.

Mmoja wa wakulima hao, Ndugu Lukasi Kauli, alitoa shukrani kwa wataalamu wa kilimo kwa kuwapelekea elimu hiyo, akisema imekuwa msaada mkubwa kwao kwani walikuwa wakikumbana na changamoto ya wadudu waharibifu bila ufumbuzi wa kitaalamu.

"Tumefurahi kupata elimu hii, hasa kuhusu matumizi sahihi ya dawa za kuua wadudu. Changamoto hii ilikuwa inatukwamisha kwa muda mrefu, lakini sasa tunaamini mavuno yetu yatakuwa bora," alisema Kauli.



Ziara hiyo ni mwendelezo wa juhudi za Halmashauri ya Wilaya ya Songea katika kuwajengea uwezo wakulima wake ili kuendeleza kilimo chenye tija na kuongeza mapato ya kaya pamoja na pato la Halmashauri.
























Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa