• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WASIRA ATIA NENO UKAMILISHAJI WA MIRADI SONGEA DC, AMPONGEZA DKT. SAMIA

Tarehe ya Kuwekwa: June 12th, 2025


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Mhe Stephen Wasira, leo Juni12, 2025 amefika Halmashauri ya Wilaya ya Songea na kukutana na viongozi mbalimbali ikiwemo wanachama wa CCM na kuwapongeza kwa mafanikio makubwa ya ukamilishaji wa miradi ya maendeleo.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo katika Shule ya Sekondari Maposeni, Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Akitaja mafanikio hayo, Mhe. Wasira alisema "Katika kipindi cha miaka minne tu, ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mheshimiwa Rais amejenga shule mpya nne za sekondari, madarasa mapya 142, zahanati 17, vituo vya afya vinne, na pia umeme umefika katika vijiji vyote vya halmashauri hii."

Katika hotuba yake, Wasira amempongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa anazoendelea kuzifanya katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi, akisema kuwa hiyo ndiyo dhana ya msingi ya Ilani ya CCM.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, alimshukuru Makamu Mwenyekiti CCM Taifa kwa kufanya ziara Mkoani humo, hususan katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, pia alituma salamu za Shukrani kwa Mhe Rais kwa miradi mingi iliyofika Mkoani Ruvuma.

"Ujio wako ni wa kipekee. Ninashukuru kwa ushirikiano mkubwa ninaoupata kutoka Chama Cha Mapinduzi katika kutekeleza majukumu yangu kwa wananchi," alisema Kanali Ahmed.

Alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mheshimiwa Jenista Mhagama, kwa kazi nzuri anayoifanya. "Mheshimiwa Jenista amekuwa akilitumikia Jimbo la Peramiho kwa moyo wa kujituma. Kila eneo alilopewa kulitumikia amelitendea haki inayostahili, na mchango wake unahisiwa ndani na nje ya mkoa huu," aliongeza.

Aidha, Ndugu Wasira aliwataka wajumbe wote walioshiriki mkutano huo kuwa mabalozi wa kudumisha na kulinda amani ya taifa, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025. "Ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha kuwa tunalinda misingi ya amani na mshikamano wa kitaifa. Amani ni msingi wa maendeleo yetu," alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Wasira alitoa shukrani za dhati kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa zawadi walizompatia. Zawadi hizo ni pamoja na fedha taslimu shilingi 150,000, mbuzi mmoja, jogoo mmoja, mahindi kilo 500, mpunga kilo 200 na maharagwe kilo 110 ambazo ziliwasilishwa kwake na Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. Mtela Mwampamba.

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali, pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • WASIRA ATIA NENO UKAMILISHAJI WA MIRADI SONGEA DC, AMPONGEZA DKT. SAMIA

    June 12, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA SONGEA AWAPONGEZA WATENDAJI WA HALMASHAURI KWA KUSIMAMIA VIZURI UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE BORA

    June 11, 2025
  • MATUMIZI YA LISHE ILIYO BORA YASISITIZWA MASHULENI

    June 10, 2025
  • KITUO CHA AFYA MATIMILA CHAKABIDHIWA GALI LA WAGONJWA.

    June 06, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa