• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

Tarehe ya Kuwekwa: June 19th, 2025


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi Elizabeth Mathias Gumbo, ametoa wito kwa wasimamizi wa miradi ya maendeleo kuhakikisha usimamizi makini na wenye tija katika utekelezaji wa miradi inayotarajiwa kuanza hivi karibuni, yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.6.

Akizungumza katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo, Gumbo aliwataka wasimamizi hao kufuata kikamilifu maelekezo waliyopewa, ikiwa ni pamoja na kuzingatia ushirikishwaji wa kamati za ujenzi katika kila hatua ya utekelezaji pamoja na kufanya manunuzi kwa kutumia Mfumo wa Kitaifa wa Manunuzi kwa Njia ya Kielektroniki (NeST).

"Ni muhimu kuhakikisha miradi hii inatekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha na kwa uwazi mkubwa, ili wananchi wapate huduma bora na ya kudumu," alisema Gumbo.

Kwa upande wake, Afisa Mipango wa Halmashauri hiyo, Ndugu Exavery Luyagaza, alipokea maelekezo hayo kwa niaba ya timu ya wasimamizi wa miradi na akaahidi kuyasimamia kikamilifu ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi unaendana na viwango vilivyowekwa, na kwamba kila hatua itasimamiwa kwa uwazi na uadilifu.

Aidha Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Flora Tairo, aliwataka wasimamizi hao kuzingatia makadirio ya ujenzi (BOQ) ili kupata majengo yenye ubora unaostahili na kuzuia upotevu wa rasilimali.

“Miradi yote itekelezwe kulingana na BOQ, ili tufikie viwango vya kitaalamu na kuepuka hasara zisizo za lazima,” alisisitiza Mhandisi Tairo.

Miradi inayotarajiwa kutekelezwa ni pamoja na Umaliziaji wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi Ndirima, Umaliziaji wa maabara katika shule za sekondari za Darajambili, Lupunga na Mhalule, Ujenzi wa madarasa na vyoo katika shule za msingi Magagura na Namakinga, Ujenzi wa vituo vya afya katika kata za Mpandangindo na Peramiho, Umaliziaji wa zahanati katika vijiji vya Morogoro, Magima na Ndongosi,  Umaliziaji wa vituo vya afya katika kata za Kilagano, Magagura na Matimila.

Utekelezaji wa miradi hii unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa huduma bora za elimu na afya kwa wananchi wa Wilaya ya Songea, na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa