• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI WA MPITIMBI WATANUFAIKA NA MRADI WA MABWAWA YA SAMAKI

Tarehe ya Kuwekwa: October 11th, 2023


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Mhe. Komredi Odo Mwisho amewataka wananchi wa Kijiji cha Mpitimbi B kutumia fursa zilizopo kujiinua kiuchumi wakati akikagua mradi wa Shamba darasa la ukuzaji wa viumbe maji mnamo tarehe9 Octoba 2023 wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya Mkoa wa Ruvuma katika Kijiji hicho cha Mpitimbi B Kata ya Mpitimbi

Akikagua ujenzi wa miundombinu hiyo ambayo ni mabwawa manne(4), chumba cha darasa la kujifunzia, vyoo matundu mawili na fensi, amesema kuwepo kwa mabwawa hayo katika Kijiji hicho kitasaidia kukuza kipato cha wananchi wa maeneo hayo pia pindi mradi huo utakapo kamilika afya za binadamu zitaimarika kutokana na samaki watakao patikana kupitia mradi huo. Ambapo amesema

" Niwapongeze sana kwa hatua hii mlioifikia nami nawambieni kupitia kukamilika kwa mradi huu hakika mtapata mafanikio makubwa na yatawafanya mkue kiuchumi tulizoea kupata samaki kutoka Ziwa Nyasa, Victoria hata Ziwa Tanganyika na bahari ya Hindi lakini sasa kupitia mradi huu mtaweza kula samaki wanaozalishwa Kijiji cha Mpitimbi hivyo hiyo kwenu ni kama fulsa ya kukua kiuchumi na hilo ndilo lengo la Raisi wetu mama yetu mpendwa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwani anakiu ya kuona kila Mtanzania ananufaika na matunda ya nchi yake"

Basi kipekee naomba nitumie fursa hii kumshukuru Mhe. Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa wananchi wa Kijiji cha Mpitimbi na kuamua kutoa fedha kwaajili ya Mradi huu ambao utaenda kuwanufaisha watu wengi sana endapo utatumika vizuri, vilevile nimshukuru Mbunge wa Jimbo la Peramiho Jenista Joakim Mhagama kwa juhudi zake katika Jimbo hili kwa kweli zinaonekana na zinazaa matunda, pia nashukuru kamati nzima ya siasa ya Mkoa wa Ruvuma kwa kumuunga mkono Raisi wetu katika kuhakikisha ilani ya Chama cha Mapinduzi inatekelezwa vyema na watu wote waliofanikisha mradi huu kuendelea na ujenzi.

Akiwasilisha taarifa ya mradi Mtendaji wa Kijiji cha Mpitimbi B Naomi Gerson amesema kwamba mradi huo ulipokea fedha kiasi cha shilingi 123,930,000 kutoka wizara ya mifugo na uvuvi kwa bajeti ya mwaka 2022/2023, ikiwa gharama za vifaa ni shilingi 104,700,000 na gharama za ufundi ni Shilingi 19,230,000 na kufanya jumla ya shilingi 123,930,000  na mradi huo unatarajiwa kugharimi jumla ya shilingi 127,000,000. Ikiwa kwa sasa mradi umefikia asilimia 97% ya ujenzi hivyo mradi upo kwenye hatua za ukamilishwaji.

Mradi huo utakapo kamilika utakuwa na mabwawa4 yenye ukubwa wa 30m x 20m x 1.5m, uzio 100m x 90m , darasa la mafunzo, stoo na choo ya matundu mawili. Pia bwawa moja linatarajiwa kuchukua vifaranga 10000 na kufanya jumla ya vifaranga 40000 kwa mabwawa yote manne.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa