• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI wa Kata ya Litisha waanza kunufaika na huduma ya maji

Tarehe ya Kuwekwa: April 22nd, 2021

WANANCHI wa Kata ya Litisha waanza kunufaika na mradi wa maji

Wanachi wa Kata ya Litisha Wilayani Songea Mkoani Ruvuma wameanza kunufaika na huduma ya mradi wa maji, mradi ulioanza kutekelezwa mwezi Mei 29 ,2020 na utakamilika Juni 30,2021

Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji taka na usafi wa mazingira Ruvuma Mhandisi Patrick Kibasa amesema mradi wa maji katika Kijiji cha Litisha ulisanifiwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 473,mpaka sasa mradi  huo umekamilika kwa asilimia 70 .

Mhandisi Kibasa amesema ujenzi wa mradi huo ni wa kisima chenye urefu wa mita 181 na kina uwezo wa kuzalisha maji lita 9,000 kwa saa ambapo amesema kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wakazi 3,226 sanjari na kuokoa muda wa wananchi ambao walikuwa wakiutumia kufuata huduma hiyo umbali mrefu.

Ameitaja miradi mingine ya maji itajengwa katika Vijiji vya Litowa,Peramiho (B) na Nakahuga kupitia mfuko wa maji wa Taifa.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji Litisha Saidi Hashimu  kwa niaba ya wananchi ameishukuru Serikali kwa kuwajengea mradi huo na kutatua changamoto  maji wakabili ikiwemo maji ambayo yatawasaidia kuongeza shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya siasa Mkoa wa Ruvuma  Oddo Mwisho ametoa wito kwa wananchi kuacha kuhujumu miundo mbinu ya maji kwa makusudi kwani kitendo hicho kinawakosesha  wananchi kupata huduma ya maji kwa uzembe wa watu wachache au mtu mmoja.

Mwisho ametoa rai kwa wananchi kulinda vyanzo vya maji ,badala yake walinde vyanzo hivyo kupanda miti rafiki ya maji ambayo itasaidia vyanzo hivyo kuwa endelevu na huduma ya maji kupatikana kwa muda wote.

Mjumbe wa Kamati hiyo ambaye pia ni  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema hatamfumbia macho mtu yoyote atakayethubutu kuharibu na kuhujumu miundo mbinu ya maji kwa sababu Serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya kujenga miradi ya maji,hivyo lazima miradi hiyo ilindwe na kutunzwa.

“Serikali itahakikisha mazingira na vyanzo vya maji vinatunzwa”,amesisitiza Mndeme

Kamati ya Siasa ya CCM mkoa wa Ruvuma imemaliza ziara ya siku tatu kukagua miradi ya maji katika wilaya za Songea na Namtumbo.

Imeandaliw na kuandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea DC

 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa