• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WANANCHI Mpitimbi wapewa rai kuwekeza mabwawa ya samaki

Tarehe ya Kuwekwa: July 15th, 2023


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho ameshauri watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Songea kuanza kutenga maeneo yatakayosaidia wananchi kujishughulisha na utengenezaji wa Mabwawa ya ufugaji wa samaki ambayo yatachochea uchumi na kuongeza wigo wa mapato kwa Halmashauri.

Kauli hiyo ameitoa wakati alipotembelea kujionea Mradi wa Shamba Darasa la Ukuzaji wa Viumbe Maji unaoendelea kujengwa na serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Kata Mpitimbi Halmashauri ya wilaya ya Songea tarehe 14/07/2023.

Waziri Mhagama ameridhishwa na hatua ya ujenzi wa shamba la darasa la ukuzaji wa viumbe hai, amesema tunaweza kutumia mabwawa ya ufugaji wa samaki kama chanzo cha ajira na uchumi kwa wananchi wa Mpitimbi B.

“Mhe. Rais, Dkt, Samia Suluhu Hassan anamaono ya mbali sana, ametupatia mradi ambao utasaidia kuzalisha mbegu na mafunzo, tunatakiwa tuanze kujiandaa kwa kutengeneza mabwawa”.

Amefafanua mradi utakapokamilika; wananchi wawe na miundo mbinu yao ya mabwawa ya ufugaji wa samaki tayari, ili mafunzo yatakapokuwa yanafanyika wawe wanachukua vifaranga na kuweka kwenye mabwawa yao, alisema Waziri Mhagama.

Tunaweza tukatumia mikopo ya Halmashauri kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kuweza kutengeneza mabwawa yao ya ufugaji wa samaki, alisisitiza.

“tunapaswa tuwe na mabwawa Mengi ya samaki kushoto na kulia mwa eneo la mradi yatakayomilikiwa na vijana wakinamama na wazee ambayo samaki watafugwa kisasa na watakuwa na uzito mzuri alisema,” Waziri Mhagama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Mhe. Menas Komba amesema Halmashauri inaanda andiko la kimkakati kwa ajili ya kupata fedha ya kuendeleza Lambo kubwa la maji lilopo katika kijiji cha Mpitimbi B ambalo linahitaji fedha Zaidi ya million 500.

Amefafanua kwamba ujenzi wa lambo hilo utaenda sambamba na Halmashauri kutaratibu kupitia Halmashauri ya kijiji maeneo ambayo wananchi watajenga mabwawa ya kufugia samaki, alisema

Awali katika taarifa Mhandisi Msimamizi wa Mradi, kutoka Halmashauri ya Songea Bi,Flora Tairo alisema Mradi uko katika hatua ya ukamilishwaji, kwa majengo na upandaji nyasi kwenye kingo za mabwawa.

Ameongeza kusema mradi utakapokamilika utakuwa na mabwawa manne, uzio, darasa la mafunzo, stoo pamoja na maliwato.

Akieleza umuhimu wa mradi Bi, Agatha Mapunda Mkazi wa Mpitimbi B amesema wanamshukuru Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mradi na wamejiandaa kupokea mafunzo

Amesema mradi utawasaidia kupata lishe bora na fursa za biashara zitakazojitokeza wakati wa uzalishaji.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa