• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

WAKULIMA WAASWA KUTUMIA MBINU SAHIHI ZA UVUNAJI WA MAHINDI ILI KUPUNGUZA HASARA

Tarehe ya Kuwekwa: June 17th, 2025


Wakulima Halmashauri ya Wilaya ya Songea, wamehimizwa kuzingatia mbinu bora za uvunaji wa mahindi ili kupunguza upotevu wa mazao na kuhakikisha ubora wa mavuno unadumu hadi sokoni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Frank Sungau, ambaye amekaimu Idara hiyo, Amesema mahindi yanapaswa kuvunwa yakiwa yamekomaa vizuri na kukauka kwa kiwango kinachotakiwa, huku dalili kuu za kukomaa zikiwa ni magunzi kuanza kuinama chini na majani ya mabua kukauka.

“Ni muhimu kuvuna mahindi mapema baada ya kukomaa ili kupunguza hasara inayoweza kutokea kutokana na kuchelewa kuvuna, hasa kipindi hiki ambacho hali ya hewa inaweza kubadilika ghafla,” alieleza Sungau.

Aidha, aliwaonya wakulima dhidi ya uuzaji holela wa mahindi kwa kushindwa kuzingatia mahitaji ya chakula kwa familia zao kwa mwaka mzima. “Kila kaya izingatie idadi ya wanachama wake, hakikishe kuna chakula cha kutosha kwa matumizi ya mwaka mzima ndipo ziada iuzwe,” alisisitiza.

Wakati huo huo, Sungau amesema kuwa Serikali imepanga kuanza rasmi ununuzi wa mahindi kwa msimu wa mwaka 2025/2026 kuanzia Julai 1, 2025 kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Songea.

Katika hatua nyingine, Halmashauri ya Wilaya ya Songea imeendelea kushika nafasi ya kwanza kwa uzalishaji wa mahindi Mkoani Ruvuma kwa zaidi ya misimu mitano mfululizo, na hivyo kuchangia Mkoa wa Ruvuma kuongoza kitaifa katika uzalishaji wa mazao ya chakula kwa zaidi ya miaka mitano.

“Ushirikiano wa karibu kati ya maafisa ugani na wakulima, pamoja na jitihada za Serikali katika kuwapatia pembejeo za ruzuku, ndiyo msingi wa mafanikio haya,” alisema Sungau.

Ameeleza kuwa Serikali imekuwa ikiwezesha wakulima kwa kuwapatia mbolea na mbegu bora kwa njia ya ruzuku, pamoja na kuwapatia maafisa ugani vitendea kazi kama pikipiki na vifaa vya kupimia udongo ili kuongeza ufanisi.

Kwa msimu ujao wa kilimo, mkakati uliowekwa ni kuongeza tija ya uzalishaji kwa kupitia mafunzo ya maafisa ugani walioko katika kata na vijiji, kupanua ukubwa wa mashamba, na kuongeza mavuno kutoka tani nne hadi tani tano kwa hekta moja.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YATINGA KWA KISHINDO UMISETA TAIFA

    June 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa