• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UZINDUZI WA JUKWAA LA WANAWAKE HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

Tarehe ya Kuwekwa: August 3rd, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Songea Ndugu Pololet Mgema amezindua jukwaa la Wanawake wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea na kuwataka kutumia jukwaa hilo kwa ajili ya kujadili fursa na changamoto zinazowakabili katika kujiletea maendeleo.

Akimkaribisha mkuu wa Wilaya ya Songea Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ndugu Simon Bulenganija amesema Jukwaa la wanawake ni muhimu kwa Ustawi na maendeleo ya jamii nzima kwani ukimkomboa mwanamke kiuchumi umekomboa jamii nzima.

Afisa maendeleo ya jamii wa wilaya bi, Judith Ngowi amesema uwezeshaji wa wanawake kiuchumi unasimamiwa kikamilifu na kamati zimeundwa kuanzia ngazi ya Taifa mpaka kijiji na pia kuna waratibu wa dawati la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kuanzia ngazi ya Taifa hadi Kata. Kauli mbiu ya mwaka huu ni  ‘’Wezesha wanawake kiuchumi ili kujenga uchumi wa kati na Tanzania ya viwanda’’

Uanzishwaji wa jukwaa la kuwawezesha  wanawake ni agizo la Mh. Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, ambaye aliteuliwa na katibu mkuu wa umoja wa mataifa kuwa Mjumbe mmojawapo wa timu ya viongozi na wataalamu ambao watafanya kazi kama chombo cha juu katika kupunguza na kuondoa pengo kubwa ambalo limejengeka Duniani na kuongeza ushiriki wa wanawake katika uchumi Duniani na kote ili kufikia maendeleo ambayo pia yamesisitiza uwezeshaji wa Wanawake Kiuchumi.

Lengo kuu la jukwaa la uwezeshaji  Wanawake kiuchumi ni kukutana pamoja na kujadili fursa, Changamoto na jinsi ya kushiriki kikamilifu katika biashara na shughuli nyingine za kiuchumi katika Wilaya. 

Vilevile kuongeza uelewa wa Wanawake katika upatikanaji wa wa Mitaji, Sheria za nchi katika masuala ya uchumi na jinsi ya kujitegemea kiuchumi. Kwani imebainika kuwa Wanawake hawapati fursa za kutosha za  kiuchumi hapa Tanzania na duniani kote. Hii inatokana na kuto kuwa na usawa katika fursa, uwezo wa kupata mitaji na ajira.

Hivyo Jukwaa hili litasaidia kuondoa matabaka na sheria kandamizi za uchumi kwa Wanawake katika kuleta maendeleo ya usawa katika pato la familia, jamii na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, KARIBU RUVUMA UJIO WAKO NI MUHIMU KWA MASLAHI YA SONGEA DC

    July 27, 2025
  • MFUMO WA NeST UMEBORESHA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KATIKA MANUNUZI YA UMMA

    July 21, 2025
  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa