• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

Tarehe ya Kuwekwa: June 20th, 2025


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, wanategemea kunufaika na ujenzi mpya wa Mradi wa Barabara ya Likuyufusi hadi Mkenda unaitarajia kuanza hivi karibuni

Akizungumza na wanachi wa Jimbo la peramiho, Mbunge wa Jimbo la Peramiho ambaye pia ni Waziri wa Afya, Mhe Jenista Mhagama, amesema mradi wa ujenzi wa barabara ya Likuyufusi–Mkenda utaleta mageuzi makubwa katika sekta ya usafirishaji, usalama wa mipaka, pamoja na shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

katika hafla ya kukabidhi rasmi kazi ya ujenzi kwa mkandarasi kutoka kampuni ya China First Highway Engineering Co. Ltd, Mhagama alisema barabara hiyo itarahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka mashambani kwenda masokoni, kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara, pamoja na kuimarisha fursa za uwekezaji kwa wakazi wa maeneo hayo.


"Ni muda wa wananchi kuongeza kasi ya uzalishaji kupitia kilimo, ufugaji na biashara ndogondogo, ili waweze kunufaika na barabara hii ambayo itakuwa mkombozi mkubwa," alisisitiza Mhagama.


Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Fedinand Mdoe, aliwahakikishia wananchi 851 waliopisha mradi kuwa watalipwa fidia stahiki kwa wakati bila kuathiri shughuli zao. Alieleza kuwa tathmini ya mali za wananchi hao imeshakamilika na kwamba zaidi ya Shilingi Bilioni 5 zimetengwa kwa ajili hiyo, ambazo zitalipwa mara baada ya TANROADS kupokea fedha kutoka Wizara ya Fedha.

Mhandisi Mdoe alibainisha kuwa mradi huo unatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa gharama ya Shilingi Bilioni 110.77, na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 27. Aidha, aliweka bayana kuwa TANROADS itasimamia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu wa kushughulikia malalamiko kupitia kamati maalum.


Halmashauri ya Wilaya ya Songea ni miongoni mwa maeneo yanayotarajia kunufaika kwa kiwango kikubwa kupitia ujenzi huo, hasa kutokana na barabara hiyo kuunganisha vijiji mbalimbali vya vijijini na miji mikubwa ya kibiashara. Mradi huo utafungua lango muhimu la kiuchumi kati ya Wilaya ya Songea na Wilaya ya Nyasa, pamoja na kuwezesha usafirishaji wa watu na bidhaa kati ya Tanzania na Msumbiji kupitia mpaka wa Mkenda.


Akizungumza kwa niaba ya serikali ya wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, alisema barabara hiyo ni kichocheo muhimu cha maendeleo kwani itahamasisha wawekezaji, kuongeza fursa za ajira, na kurahisisha huduma za kijamii kufika kwa wananchi kwa urahisi. Alisisitiza kuwa ni wajibu wa viongozi na watendaji kuwapa wananchi taarifa za kutosha kuhusu miradi kama hii ili kuimarisha uhusiano kati ya serikali na jamii.


Wananchi wa kijiji cha Litapwasi, miongoni mwa vijiji vinavyonufaika na mradi huo, wameonyesha matumaini makubwa ya kupungua kwa changamoto ya usafiri hasa wakati wa mvua na kiangazi. Bali Tindwa na Felista Luena ni miongoni mwa wakazi waliotoa shukrani kwa serikali kwa kuona hatua ya mradi kuanza rasmi, wakisema kuwa sasa wanaamini ahadi ya maendeleo inatekelezwa kwa vitendo.


Awamu ya kwanza ya mradi huo inajumuisha ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 60 kutoka Likuyufusi hadi Mkayukayu, huku awamu inayofuata ikitarajiwa kuendelea kutoka Mkayukayu hadi Mkenda (km 64), pamoja na ujenzi wa madaraja ya Mitomoni na Mkenda.


Mradi huu mkubwa unatarajiwa kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo katika Ukanda wa Kusini, hasa kwa Wilaya ya Songea ambayo sasa inachipua kama kitovu kipya cha biashara, kilimo na usafirishaji mkoani Ruvuma.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YATINGA KWA KISHINDO UMISETA TAIFA

    June 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa