• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UFUTA wawaingizia wakulima Songea milioni 400

Tarehe ya Kuwekwa: June 16th, 2020

Wakulima wa Songea wagomea bei mnada wa soya

Waingiza milioni 400 katika ufuta

MNADA wa nane wa mazao ya ufuta na soya ulioshirikisha Halmashauri tano za Mkoa wa Ruvuma na vyama vya msingi vya ushirika 11 umewawezesha wakulima kuuza kilo zaidi ya 264,000 za ufuta na kuwaingizia zaidi ya milioni 400.

Akizungumza mara baada ya kufanyika mnada huo katika soko la mazao la Lilambo,Meneja Operesheni wa Chama Kikuu cha Ushirika wa mazao ya kilimo Songea na Namtumbo (SONAMCU) Zamakanary Komba amezitaja Halmashauri tano zilizoshiriki katika mnada wa zao la ufuta kuwa ni Halmashauri ya Mbinga, Halmashauri ya Songea,Madaba na Nyasa.

Amevitaja vyama 11 vilivyoshiriki katika mnada huo kuwa ni Kingambi,Tingi,Kilumba,Mpiki,Lina,MugisoNalisi,Songea West, Amkeni, Muungano na Tama na kwamba katika kilo za ufuta zilizouzwa katika mnada huo,bei ya juu iliyokubalika na wakulima ilikuwa ni sh.1930 na baada ya kutoa tozo mkulima anauza kwa  sh.1759.

“Pesa ambayo imekwenda moja kwa moja kwa wakulima katika mnada wa leo ni  shilingi milioni 465,250,223,lakini kabla ya makato  kwenda kwa wakulima,fedha ilikuwa ni zaidi ya  milioni  510’’,alisisitiza Komba.

Komba amesema kupitia mnada huo, tozo ya mfuko wa maendeleo katika Halmashauri imepatikana shilingi milioni 7.9 na kwamba ushuru wa Halmashauri  ni zaidi ya sh. Milioni 20.6.

Hata hivyo katika mnada wa zao la soya ambao umeshirikisha Halmashauri mbili   wakulima wamegomea bei ya zao hilo ambayo bei ya juu ilikuwa ni  680 kwa kilo ambapo ukitoa tozo mkulima alikuwa anabakiwa na sh.558.

“Wakulima wa soya wamegomea bei hiyo kwa hiyo tumeusogeza mbele mnada huo hadi Jumatatu ijayo,leo tuliangalia asubuhi bei ya Dar es salaam ilikuwa kilo ni sh.800,Morogoro sh.850 kwa hiyo tunawashauri wenye Kampuni wanunue bei nzuri kutoka kwa wakulima’’,alisisitiza Komba.

Wakulima wa zao la ufuta katika Wilaya za Namtumbo,Songea na Tunduru mkoani Ruvuma wameanza kunufaika na zao hilo baada ya kupokea shilingi bilioni 16.8 tangu kuanza kuuza zao hilo kwa mfumo wa stakabadhi ghalani Apirili  mwaka huu

Imeandikwa na Jacquelen Clavery

Afisa Habari Songea DC

Juni 15,2020 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa