• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

TAKUKURU MKOANI RUVUMA YAWATAKA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2020.

Tarehe ya Kuwekwa: July 16th, 2020

Ruvuma imewataka Wananchi kutoa ushirikiano katika kudhibiti vitendo vya rushwa katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 2020.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Kamanda waTAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Bw Owen Ajasson wakati akitoa taarifa ya Utendaji  kazi wa TAKUKURU kwa kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni 2020 katika  ofisi za TAKUKURU  leo.

Ajasson amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Ruvuma kutoa Ushirikiano wa kudhibiti vitendo vya rushwa kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa vitakavyo fanywa na wagombea mbalimbali kwa nafasi za  Udiwani na Ubunge pamoja na wapambe wao.

“TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma tumejipanga kufuatilia kwa ukaribu mienendo ya wagombea na kampeni zao na wapambe wao ili kuzuwia na kupambana na Rushwa” Alisema Ajasson.

Amesema Katika kipindi cha miezi mitatu Taasisi hiyo imefanikiwa kukokoa kiasi cha fedha zaidi ya  Sh. Milioni 359 kutoka vyama vya Ushirika (SACCOS), kwa Wilaya ya Songea, Mbinga, na Namtumbo, Makusanyo ya Vitambulisho ya wafanyabiashara wadogowadogo (wamachinga) kwa Wilaya ya Tunduru, Mbinga, na Halmashauri ya Wilaya ya Songea katika kijiji cha Makwaya kata ya Muhukuru- Lilahi, na maeneo mengine ni Sekta ya Elimu, Benki ya Wananchi Mbinga, na Ubadhilifu wa Makusanyo yatokanayo na  POS pamoja na dhuluma dhidi ya wakulima wa zao la korosho.

Ameongeza kwa kusema katika kipindi tajwa Taasisi hiyo imefanya ufuatiliaji wa miradi  8 ya maendeleo  ambayo ni ujenzi wa Miundombinu na afya yenye zaidi ya thamani ya sh. bilioni moja na milioni mia nane miradi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea na maeneo mengine ikiwemo  ujenzi wa kituo cha afya Magagura na Matimira na matengenezo ya Barabara ya Maposeni hadi Likingo unaosimamiwa na TARURA.

Ajasson amesema Katika ukaguzi wa Mradi wa matengenezo ya Barabara ya Maposeni hadi Likingo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea ilibainika kwamba alama za Barabarani katika barabara hiyo hazijawekwa na kipande cha kiliometa 3 ambacho kilitakiwa kiwekewe kifusi hakijawekewa.

TAKUKURU kwa kipindi cha Julai- Septemba imejipanga kuendelea kuelimisha wananchi kupiga vita vitendo vya  rushwa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika mwezi oktoba 2020 ili wasikubali kurubuniwa kwa vitendo vya Rushwa na kutambua haki na wajibu wao wa kufahamu Uchaguzi ninini, lengo la Uchaguzi, sheria inayoongoza uchaguzi pamoja na umuhimu wa kupiga kura.

IMEANDIKWA NA;

JACQUELEN CLAVERY

16.07.2020

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa