• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma imefanya ufuatiliaji wa miradi inayogharimu kiasi cha zaidi ya Bilioni 6

Tarehe ya Kuwekwa: November 30th, 2022

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Ruvuma kwa kipindi cha miezi mitatu imefanya ufuatiliaji wa miradi iliyogharimu kiasi cha fedha Zaidi ya shilingi Bilioni 6.

Hayo yamethibitishwa na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Janeth Haule wakati akitoa taarifa ya utendaji kazi wa ofisi kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Julai hadi Septemba 2022 kwa waandishi wa habari.

Akizungumza katika kikao hicho amesema ufuatiliaji huo umefanyika katika miradi ya ujenzi wa barabara Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwa thamani ya Bilioni 5,764,392,899.80 na nyumba za Watumishi Wilayani Tunduru na Nyasa zenye thamani ya Shilingi Milioni 125,000,000 pamoja na ujenzi wa shule mpya ya sekondari Wilayani Tunduru wenye thamani ya Shilingi Milioni 470,000,000.

Naibu Mkuu wa TAKUKURU Janeth ameongeza kuwa lengo la ufuatiliaji huo ni kuhakikisha kuwa miradi yote ya Serikali inatekelezwa kwa wakati ikiwa na ubora unaolingana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Vilevile amesema TAKUKURU imedhamiria kuendelea kufanya kazi za uzuiaji rushwa kwa lengo la kubaini mianya ya rushwa katika maeneo mbalimbali zikiwemo Taasisi za Umma na Binafsi na kushauri namna bora za kuiziba mianya hiyo.

Hata hivyo ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma kuendelea kutoa ushirikiano wa hali ya juu wakati wa kutekeleza miradi ya mpango wa maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya Uviko-19 katika Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa pindi utakapohitajika.

Janeth amesema kwa mujibu wa kifungu cha 7 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na 11 ya mwaka 2007, TAKUKURU ina majukumu makuu matatu ambayo ni kuelimisha jamii juu ya rushwa na madhara yake, kufanya chambuzi za mifumo kwenye taasisi za umma na sekta binafsi pamoja na kufanya uchunguzi na kufikisha watuhumiwa mahakamani kwa kibali cha Mkurugenzi wa mashtaka baada ya chunguzi hizo kukamilika.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa