• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC YATOA MAFUNZO KWA VIKUNDI 83 VILIVYONUFAIKA NA MKOPO WA ASILIMIA 10

Tarehe ya Kuwekwa: December 24th, 2025


Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii leo Desemba 23, 2025 imetoa mafunzo kwa jumla ya vikundi 83 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, ambapo jumla ya vikundi 45 vya wanawake, vikundi 30 vya vijana na vikundi 8 vya watu wenye ulemavu vimenufaika na mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 726.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea ambaye pia ni Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Bi. Zawadi Nyoni, amewataka wanufaika hao kudumisha upendo, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wanakikundi ili kuhakikisha miradi wanayoitekeleza inaleta tija na mikopo inarejeshwa kwa wakati.

Bi. Zawadi amesisitiza kuwa fedha zilizotolewa zitumike kwa kuzingatia mchanganuo uliowasilishwa wakati wa kuomba mkopo, pamoja na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha. Aidha, amewahimiza wanufaika kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwawezesha wananchi wengine nao kunufaika, akisisitiza kuwa “dawa ya deni ni kulipa.”

Katika mafunzo hayo, elimu mbalimbali zilitolewa kulingana na aina ya miradi inayotarajiwa kutekelezwa na vikundi hivyo. Akitoa elimu ya kilimo, Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Leonard Mhagama, amewahimiza wanufaika wanaojihusisha na shughuli za kilimo kufanya uchaguzi sahihi wa mashamba, kutumia mbegu bora, kusafirisha pembejeo kwa wakati na kufuata kanuni na taratibu bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kuhakikisha marejesho ya mikopo yanafanyika kwa wakati.


Kwa upande wa vikundi vya vijana vilivyopanga kutumia mikopo hiyo kununua pikipiki kwa ajili ya biashara ya bodaboda, Afande Ramadhan Duru ametoa elimu ya usalama barabarani, akisisitiza umuhimu wa kuwa na leseni halali ya udereva, kuzingatia sheria za barabarani na kutunza vyombo vya moto ili kudumisha biashara na kuhakikisha marejesho ya mikopo yanaendelea vizuri.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

    January 13, 2026
  • MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

    January 11, 2026
  • WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 09, 2026
  • MWAMPAMBA AIPONGEZA SONGEA DC NA KUSISITIZA MIKOPO YA 10% IENDELEE KUTOLEWA.

    January 08, 2026
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa