• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TSH MILIONI 30 KITUO CHA AFYA MUHUKURU LILAHI

Tarehe ya Kuwekwa: November 20th, 2025


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Louis Chomboko, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, leo Novemba 20, 2025, amepokea jumla ya vitanda 25, magodoro 25 na mashuka 50 kutoka kwa Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) katika Kituo cha Afya cha Muhukuru Lilahi.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano, Dkt. Chomboko ameishukuru taasisi hiyo kwa kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuiendeleza sekta ya afya, hususani kwa kuleta msaada huo katika kituo hicho kinachohudumia wananchi wa maeneo hayo.

“Binafsi napenda kuwashukuru sana PSSSF kwa kuona umuhimu wa afya za wananchi. Najua vituo ni vingi na mahitaji ni makubwa kila mahali, lakini mmeona ni vyema kuunga mkono kituo hiki ambacho kilikuwa na uhitaji mkubwa, Tunawashukuru sana,” alisema Dkt. Chomboko.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Lulyalya Sayi, amesema pamoja na mfuko huo kuwa mpya, umefanikiwa kutoa huduma na misaada kwenye maeneo mbalimbali yenye mahitaji makubwa, na leo umefika Muhukuru Lilahi ili kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya.

“Tunaamini vifaa hivi vitawasaidia wananchi wengi, wakiwemo watumishi wa umma ambao ni wanachama wetu, pamoja na wananchi wengine wa kawaida. Sisi kama mfuko tunaunga mkono jitihada za Mhe. Rais zinazolenga kazi na utu, Wananchi wakitibiwa na kuwa na afya njema, wataweza kufanya kazi ipasavyo,” alisema Bw. Sayi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bw. Hassan Mtamba, akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Halmashauri, ameishukuru PSSSF kwa kuichagua Songea DC miongoni mwa Halmashauri nyingi za Mkoa huo.

“Tunawashukuru sana kwa msaada huu mkubwa, tunaamini Halmashauri ni nyingi katika Mkoa huu, lakini mmeliona jicho la huruma kufikisha msaada hapa Songea DC. Tunaahidi vifaa hivi tutavitunza na kuvifanya vitumike kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuwanufaisha wananchi,”

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • FAHAMU KUHUSU BARAZA LA MADIWANI; MUUNDO NA UTENDAJIKAZI WAKE

    November 25, 2025
  • SONGEA DC, YATEMBELEA MIKOA INAYOLIMA KAHAWA KWA LENGO LA KUPATA UZOEFU

    November 19, 2025
  • DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI YA SONGEA KWA KUIMARISHA HALI YA LISHE, ATOA WITO WA KUENDELEZA JITIHADA

    November 17, 2025
  • SONGEA DC YAPOKEA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA TSH MILIONI 30 KITUO CHA AFYA MUHUKURU LILAHI

    November 20, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa