• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONGEA DC YAENDESHA MAFUNZO YA MABORESHO YA MFUMO WA FFARS KWA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA

Tarehe ya Kuwekwa: August 24th, 2025


Mafunzo ya maboresho ya mfumo wa Uhasibu na Utoaji Taarifa za Fedha kwa Vituo vya Kutolea Huduma (FFARS) yamefanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, yakihusisha wahasibu kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.



Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Onesmo Kabuga, ambaye aliwataka washiriki kuyapokea kwa moyo wa uwajibikaji maboresho hayo ya mfumo. Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuboresha mfumo wa manunuzi na usimamizi wa fedha katika vituo vya kutolea huduma, hatua itakayosaidia kuongeza uwazi na ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma.


Akizungumza wakati wa ufunguzi, Ndugu Kabuga alieleza kuwa mfumo huo utasaidia kupunguza matumizi makubwa ya karatasi, kuokoa muda pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji. “Kupitia maboresho haya, shughuli nyingi za kifedha zitafanyika moja kwa moja kwenye mfumo, jambo litakalorahisisha upatikanaji wa taarifa na kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi wetu,” alisema.

Mafunzo hayo pia yalihudhuriwa na wakufunzi wa maudhui ya mfumo huo, akiwemo Ndugu Lameck Mkongogo, Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambaye aliwafundisha washiriki namna ya kutumia maboresho hayo kwa vitendo. Alisisitiza kuwa mfumo huo utarahisisha ufuatiliaji wa fedha katika kila kituo na hivyo kuongeza uwajibikaji. Washiriki wa mafunzo hayo walitoka shule za msingi na sekondari, hospitali, vituo vya afya, zahanati pamoja na vijiji,



Washiriki wa mafunzo hayo walionesha mwitikio chanya kwa maboresho ya mfumo wa FFARS, wakieleza kuwa utarahisisha utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati. Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha kuwa mifumo ya kidijitali inatumika ipasavyo katika kusimamia fedha za umma ili kuchochea maendeleo endelevu kwa wananchi.







































Songea DC yaendesha mafunzo ya maboresho ya mfumo wa FFARS kwa vituo vya kutolea huduma



Mafunzo ya maboresho ya mfumo wa Uhasibu na Utoaji Taarifa za Fedha kwa Vituo vya Kutolea Huduma (FFARS) yamefanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, yakihusisha wahasibu kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.



Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Onesmo Kabuga, ambaye aliwataka washiriki kuyapokea kwa moyo wa uwajibikaji maboresho hayo ya mfumo. Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuboresha mfumo wa manunuzi na usimamizi wa fedha katika vituo vya kutolea huduma, hatua itakayosaidia kuongeza uwazi na ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma.



Akizungumza wakati wa ufunguzi, Ndugu Kabuga alieleza kuwa mfumo huo utasaidia kupunguza matumizi makubwa ya karatasi, kuokoa muda pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji. “Kupitia maboresho haya, shughuli nyingi za kifedha zitafanyika moja kwa moja kwenye mfumo, jambo litakalorahisisha upatikanaji wa taarifa na kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi wetu,” alisema.



Mafunzo hayo pia yalihudhuriwa na wakufunzi wa maudhui ya mfumo huo, akiwemo Ndugu Lameck Mkongogo, Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambaye aliwafundisha washiriki namna ya kutumia maboresho hayo kwa vitendo. Alisisitiza kuwa mfumo huo utarahisisha ufuatiliaji wa fedha katika kila kituo na hivyo kuongeza uwajibikaji. Washiriki wa mafunzo hayo walitoka shule za msingi na sekondari, hospitali, vituo vya afya, zahanati pamoja na vijiji,



Washiriki wa mafunzo hayo walionesha mwitikio chanya kwa maboresho ya mfumo wa FFARS, wakieleza kuwa utarahisisha utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati. Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha kuwa mifumo ya kidijitali inatumika ipasavyo katika kusimamia fedha za umma ili kuchochea maendeleo endelevu kwa wananchi.



































Songea DC yaendesha mafunzo ya maboresho ya mfumo wa FFARS kwa vituo vya kutolea huduma



Mafunzo ya maboresho ya mfumo wa Uhasibu na Utoaji Taarifa za Fedha kwa Vituo vya Kutolea Huduma (FFARS) yamefanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, yakihusisha wahasibu kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.



Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Onesmo Kabuga, ambaye aliwataka washiriki kuyapokea kwa moyo wa uwajibikaji maboresho hayo ya mfumo. Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuboresha mfumo wa manunuzi na usimamizi wa fedha katika vituo vya kutolea huduma, hatua itakayosaidia kuongeza uwazi na ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma.



Akizungumza wakati wa ufunguzi, Ndugu Kabuga alieleza kuwa mfumo huo utasaidia kupunguza matumizi makubwa ya karatasi, kuokoa muda pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji. “Kupitia maboresho haya, shughuli nyingi za kifedha zitafanyika moja kwa moja kwenye mfumo, jambo litakalorahisisha upatikanaji wa taarifa na kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi wetu,” alisema.



Mafunzo hayo pia yalihudhuriwa na wakufunzi wa maudhui ya mfumo huo, akiwemo Ndugu Lameck Mkongogo, Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambaye aliwafundisha washiriki namna ya kutumia maboresho hayo kwa vitendo. Alisisitiza kuwa mfumo huo utarahisisha ufuatiliaji wa fedha katika kila kituo na hivyo kuongeza uwajibikaji. Washiriki wa mafunzo hayo walitoka shule za msingi na sekondari, hospitali, vituo vya afya, zahanati pamoja na vijiji,



Washiriki wa mafunzo hayo walionesha mwitikio chanya kwa maboresho ya mfumo wa FFARS, wakieleza kuwa utarahisisha utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati. Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha kuwa mifumo ya kidijitali inatumika ipasavyo katika kusimamia fedha za umma ili kuchochea maendeleo endelevu kwa wananchi.





































Songea DC yaendesha mafunzo ya maboresho ya mfumo wa FFARS kwa vituo vya kutolea huduma



Mafunzo ya maboresho ya mfumo wa Uhasibu na Utoaji Taarifa za Fedha kwa Vituo vya Kutolea Huduma (FFARS) yamefanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, yakihusisha wahasibu kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea.



Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Onesmo Kabuga, ambaye aliwataka washiriki kuyapokea kwa moyo wa uwajibikaji maboresho hayo ya mfumo. Alisisitiza kuwa maboresho hayo yanalenga kuboresha mfumo wa manunuzi na usimamizi wa fedha katika vituo vya kutolea huduma, hatua itakayosaidia kuongeza uwazi na ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma.



Akizungumza wakati wa ufunguzi, Ndugu Kabuga alieleza kuwa mfumo huo utasaidia kupunguza matumizi makubwa ya karatasi, kuokoa muda pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji. “Kupitia maboresho haya, shughuli nyingi za kifedha zitafanyika moja kwa moja kwenye mfumo, jambo litakalorahisisha upatikanaji wa taarifa na kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi wetu,” alisema.



Mafunzo hayo pia yalihudhuriwa na wakufunzi wa maudhui ya mfumo huo, akiwemo Ndugu Lameck Mkongogo, Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambaye aliwafundisha washiriki namna ya kutumia maboresho hayo kwa vitendo. Alisisitiza kuwa mfumo huo utarahisisha ufuatiliaji wa fedha katika kila kituo na hivyo kuongeza uwajibikaji. Washiriki wa mafunzo hayo walitoka shule za msingi na sekondari, hospitali, vituo vya afya, zahanati pamoja na vijiji,



Washiriki wa mafunzo hayo walionesha mwitikio chanya kwa maboresho ya mfumo wa FFARS, wakieleza kuwa utarahisisha utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati. Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Songea kuhakikisha kuwa mifumo ya kidijitali inatumika ipasavyo katika kusimamia fedha za umma ili kuchochea maendeleo endelevu kwa wananchi.






























Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa