• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SONDEA DC YATAMBULISHA MIRADI YA MAENDELEO KATA YA PERAMIHO

Tarehe ya Kuwekwa: August 29th, 2025


Kaimu Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Prisila Massay, akiambatana na wataalamu wa Halmashauri hiyo, leo Agosti 29, 2025 ametembelea Kata ya Peramiho kwa ajili ya kutambulisha miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya cha Peramiho na ujenzi wa madarasa pamoja na matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi Mnyonga, kijiji cha Nguvumoja.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara, Bi. Massay amewataka wananchi wa kata hiyo kushirikiana kikamilifu katika utekelezaji wa miradi hiyo kwa kuwa itahudumia vijiji vyote vya Peramiho A, Peramiho B, Lundusi na Nguvumoja.


Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu Msingi, Mwl. Sothery Nchimbi, amesisitiza mshikamano kati ya kamati za ujenzi na wananchi, akisema mchango wa nguvu kazi za wananchi ni nguzo muhimu ya kufanikisha miradi hiyo. Ameeleza pia  ni vyema kuwatumia mafundi wazawa ili kuimarisha ubora wa kazi na kuongeza uwajibikaji, lakini kwa sharti la kuwa na vigezo vinavyohitajika kisheria ikiwemo kujisajili kwenye mfumo wa NeST.


Naye Mhandisi Hafidhi Kimaro kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea amesema kituo cha afya kitajengwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi  ya milioni 641 na kitahusisha majengo ya mama na mtoto, maabara ya kisasa, chumba cha upasuaji, jengo la kufulia, jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na vyoo.

Aidha, katika Shule ya Msingi Mnyonga, ambayo inahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum, ujenzi utahusisha madarasa mapya mawili, matundu ya vyoo 12 na ukarabati wa shule kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 131  na ujenzi wa vyoo vingine 21, kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 49.

Kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Peramiho, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nguvumoja, Ndugu Lukasi Mselewa, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea miradi hiyo yenye manufaa makubwa kwa wananchi, akisisitiza kuwa itasogeza karibu huduma za afya na elimu kwa wakazi wa eneo hilo.


Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu na kuanza kutoa huduma kufikia mwezi Januari mwakani.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa