• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Siku ya Mtoto wa Afrika: “Songea Dc yalenga kuboresha mazingira ya makuzi bora kwa mtoto kijamii, kielimu na kiafya"

Tarehe ya Kuwekwa: June 16th, 2025


Leo Halmashauri ya Wilaya ya Songea inaungana na Watanzania na jamii ya Afrika kwa ujumla kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika, ikiwa ni siku ya kutafakari, kukumbuka na kuchukua hatua juu ya ustawi wa mtoto wa kiafrika.

Katika kuadhimisha siku hii muhimu, Halmashauri ya Wilaya ya Songea inatambua kwa dhati mchango na nafasi ya watoto katika ujenzi wa jamii imara na endelevu. Watoto ni kundi linalopaswa kulindwa, kuelimishwa, na kupewa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa. Kwa kulitambua hilo, Halmashauri imeendelea kutekeleza mipango mbalimbali inayolenga kuboresha mazingira ya makuzi bora kwa mtoto kijamii, kielimu na kiafya.

Akitoa ufafanuzi Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Bi Zawadi Nyoni akiwa Ofisi kwake amesema, "Halmashauri imefanikiwa kuimarisha Kamati za Ulinzi wa Mtoto kuanzia ngazi ya vijiji hadi kata, ambazo zimekuwa mstari wa mbele katika utoaji wa elimu ya haki za watoto, uzuiaji wa ukatili, pamoja na kuratibu msaada wa kisheria kwa watoto walioko katika mazingira hatarishi. Aidha, jitihada za kuandikisha watoto wote katika elimu ya awali na msingi zimeendelea kupewa kipaumbele, huku ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya shule ukiimarishwa kila mwaka".

Pia ameeleza kuwa katika sekta ya afya, Halmashauri imehakikisha upatikanaji wa huduma muhimu za afya kwa watoto, ikiwemo chanjo, matibabu ya msingi, na huduma za lishe bora katika vituo vya afya vya serikali. Pia, kupitia programu maalum mashuleni, watoto wamekuwa wakifundishwa stadi za maisha, ujasiri, na umuhimu wa kujitambua mapema ili waweze kuwa viongozi na raia wema wa baadae.

Katika hatua nyingine Bi Zawadi ametoa wito kwa wazazi, walezi, jamii nzima na taasisi zote kuhakikisha kuwa mtoto anapewa haki yake ya msingi haki ya kuishi, kupata elimu, kulindwa dhidi ya ukatili, na kushiriki katika masuala yanayomhusu. "Ulinzi wa mtoto si jukumu la serikali pekee, bali ni wajibu wa kila mmoja wetu katika nafasi aliyonayo".

Tukiwa tunakumbuka historia ya watoto wa Soweto, ni lazima tuiangazie Songea ya leo kwa jicho la matumaini. Mtoto wa Songea ana haki ya kuota ndoto, kujifunza kwa amani, na kukua katika mazingira ya heshima na upendo. Tuendelee kushirikiana kuhakikisha kuwa hakuna mtoto anayebaki nyuma katika safari ya maendeleo.

Kwa pamoja, tuijenge Tanzania mpya kupitia watoto wetu, Siku hii ya mtoto wa Afrika imebeba kauli mbiu isemayo "Haki za Mtoto, Tulipotoka, Tulipo na Tuendako"

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YATINGA KWA KISHINDO UMISETA TAIFA

    June 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa