• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SHULE ZA SEKONDARI SONGEA DC ZAPONGEZWA, WALIMU WAAHIDI KUENDELEA KULIPA DENI LA MAFANIKIO

Tarehe ya Kuwekwa: September 4th, 2025


Matokeo mazuri ya kidato cha sita mwaka 2025 bado yanaendelea kutazamwa kama kielelezo cha mshikamano mzuri kati ya walimu, wanafunzi, jamii na Serikali kwa ujumla katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Bi Elizabeth Gumbo akitoa vyeti vya pongezi pamoja na fedha taslimu kwa shule tatu za sekondari ambazo zinatoa elimu ya kidato Cha Tano na sita kama motisha na kuwataka walimu hao kuongeza juhudi zaidi katika ufundishaji ili kuleta matokeo bora zaidi kwa mitihani ijayo. 


Ili kuunga mkono jitihada hizo, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kikiongozwa na Mkuu wa Kitengo hicho, Ndugu Augustine Nongwe, kilifanya ziara katika shule tatu za sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Songea zinazofundisha kidato cha tano na sita ambazo ni Mpitimbi, Maposeni, na Jenista Mhagama.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Mpitimbi, Mwalimu Patrick Matembo, alisema, “Ushirikiano wa karibu kati ya serikali, walimu, jamii na wanafunzi wenyewe ndiyo siri kubwa iliyotuwezesha kupata matokeo mazuri katika mtihani wa kidato cha sita mwaka 2025, Serikali kupitia kutujengea majengo na vifaa bora, pamoja na motisha kutoka kwa Mkurugenzi, imetuwezesha kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha tunapata matokeo chanya.”

Aidha, aliongeza kuwa walimu wa shule hiyo wamekuwa wakijitoa kwa dhati kumaliza mada kwa wakati na kutoa mazoezi ya mara kwa mara, huku jamii ikisaidia kudumisha nidhamu ya wanafunzi.

“Tunalo deni kwa Mkurugenzi wetu na kwa jamii inayotuzunguka, Tunaahidi kuendelea kujipanga vyema na kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi katika matokeo yajayo,” alisisitiza Mwalimu Matembo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Maposeni, Mwalimu Dismass Nchimbi, naye alisema shule yake imefanikiwa kutokana na nidhamu, mshikamano wa walimu, na juhudi za wanafunzi wenyewe.


“Tumekuwa na utaratibu wa kufuatilia kwa karibu maendeleo ya wanafunzi wetu, kutoa mitihani ya mara kwa mara, kufanya mitihani ya kikanda na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata msaada pale anapokwama, hii imekuwa nguzo muhimu ya mafanikio yetu,” alisema
























Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa