• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

SHIRIKA la PADI kuanza kutoa mafunzo kwa watoto wa kiume kupinga ukatili wa kijinsia

Tarehe ya Kuwekwa: September 10th, 2020

SHIRIKA la PADI kuanza kutoa mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto wakiume

Shirika lisilokuwa la kiserika la kuhudumia watu wasiojiweza na wenye Ulemavu ( PADI) linatarajia kuanza kutoa mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kiume wenye umri wa miaka tisa hadi 14 katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Meneja mradi  Gifti Kilasi amesema kupitia mradi wa USAID KIZAZI KIPYA unaosimamiwa na PADI utaanza kutoa mafunzo kwa watoto hao ili waweze kufahamu madhara ya ukatili wa kijinsia na waanze kupinga ukatili huo katika jamii.

Amesema mafunzo hayo yatasaidia kuandaa Taifa la vijana   wakiume wenye   maadili  mema , kuondoa migogoro, kupambana na kupinga matendo maovu ya ukatili  wa kijinsia sambamba na kuongeza upendo na mshikamano katika jamii

“Matendo mengi ya ukatili wa kijinsia yanasababiashwa na wanaume”,amesema Kilasi.

Kilasi amesema wamegeukia kundi hilo kwasababu ni kundi ambalo ni wahanga wa ukatili wa kijinsi,na kundi ambalo lilisahaulika katika kuwapa elimu ya kupambana na ukatili wa kijinsia ukilinganisha na watoto wa kike.

Afisa Ustawi wa Halmashauri ya Wilaya ya songea Suzana Mkondya amewaasa wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwasadikisha watoto wakiume kuwa majasiri ,kwani hali hiyo ni kikwazo kwa watoto wakiume kutambua madhara ya ukatili wa kijinsia na kutoa taarifa pale wanapofanyiwa vitendo hivyo katika jamii.

“Wewe ni mtoto wa kiume  kuwajasiri”,amesema Mkondya.

Amesema baada ya mafunzo hayo wanatarajia vitendo vingi vitaripotiwa katika vyombo vya dola na kutolea maamuzi ya kisheria,hata hivyo  siku zitakavyo zidi kwenda mbele matendo hayo yatapungua kwa kiasi kikubwa na watoto wataelika na kuanza kutoa elimu kwa vijana wengine.

Ameongeza kwakusema mafunzo hayo yatatolewa kwa nadharia na vitendo kupiti michezo na yatafundishwa na walimu wa shule za msingi katika maeneo  husika,pia watoto watapata fursa ya kupima magonjwa endapo watapatikana na matatizo ya kiafya hasa vvu.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Zena Ibrahimu ametoa wito kwa wadau wa mradi huo kusimamia vizuri na kutoa ushirikiano wa dhati katika utekelezaji wa mradi huo ili uweze kutoa matokeo chanya ya kujenga na kulinda maadili mema Yakitanzania.

Mradi huo utaanza  kutekelezwa Oktoba  mwaka huu tayari  wameshasajili watoto 2700 wa shule za Msingi na lengo ni kuwa fikikia watoto 8000 hadi kufikia mwezi Septemba 2021 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Watoto  katika zoezi hilo watapatikana kutoka  katika Kata ya Parangu,Maposeni,Kilagano,Litapwasi,Mpitimbi,Kizuka,Litisha na kata nyingine ni Magagara,Peramiho na Mbinga mhalule,kwakila kata zimechaguliwa shule tatu mradi wa USAID KIZAZI KIPYA umeanza kutekelezwa mwaka 2017 na utafikia mwisho wake mwezi Septemba  2020

Imeandikwa na Jacquelen Clavery

Afisa habari songea dc

Septemba  10,2020

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa