• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RUWASA kutumia bilioni 600 kusambaza maji vijijini

Tarehe ya Kuwekwa: November 22nd, 2022

MKURUGENZI Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mhandisi Clement Kivegalo amesema RUWASA inatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 600 kusambaza maji vijijini.

Amesema hayo baada ya kukagua mradi wa maji katika Kijiji cha Lipaya Halmashauri ya Songea mkoani Ruvuma katika ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya maji inayotekelezwa na RUWASA.

Amesema kutokana na utekelezaji mzuri wa miradi ya maji, Benki ya Dunia imeridhia kuongeza fedha Dola milioni 300 za Marekani ambazo ni sawa na zaidi ya shilingi bilioni 600 zote zinakwenda kuboresha maji vijijini.

Ameahidi mradi wa maji Lipaya unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni moja unatarajia kuanza kutoa maji kabla ya Desemba 30 mwaka huu ili kuwawezesha wananchi kupata maji safi na salama.

“Shida ya maji kwa utamaduni wa Afrika wanaumia zaidi ni akinamama kwa sababu wao ndiyo wanakwenda kutafuta maji,sisi kwetu RUWASA uwepo wa Rais Mama umesababisha bajeti ya fedha kuwa kubwa hivyo kuweza kutekeleza miradi mingi ya maji ndani ya muda mfupi’’,alisisitiza Mhandisi Kivegalo.

Amempongeza Meneja wa RUWASA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Rebman Ganshonga kwa kusimamia na kutekeleza vizuri miradi ya maji hali iliyosababisha kuongezewa bajeti ya miradi ya katika Mkoa wa Ruvuma toka bilioni saba hadi kufikia bilioni 11.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Jenista Mhagama amewapongeza RUWASA kwa juhudi wanazofanya za kuhakikisha wanamaliza kero ya maji maeneo ya vijijini likiwemo Jimbo la Peramiho.

Amesema katika historia ya Jimbo la Peramiho hii ni mara ya kwanza kwa timu nzima kutoka RUWASA makao makuu kufika kukagua utekelezaji wa miradi ya maji na ile yenye changamoto kuitafutia ufumbuzi ili wananchi wapate maji safi.

Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA akiwa na watendaji wakuu toka makao makuu yupo mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maji na miradi yenye changamoto kuipatia ufumbuzi ili wananchi waanze kunufaika na upatikanaji wa maji safi na salama.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Pololet Mgema amesema Mkoa wa Ruvuma una kila sababu ya kumshukuru Rais kwa kuupiga mwingi kutokana na kutoa fedha za kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ikiwemo miradi ya maji.

“Kuna watu wakisikia wananchi na viongozi wanamshukuru na kumsifia Rais wetu kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya kwa watanzania wanakasirika,sisi tunaotambua kazi yake tunasema anaupiga mwingi’’,alisema.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa