• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RC RUVUMA AFANYA ZIARA YA KIKAZI, AKAGUA MIRADI MITATU YA ELIMU SONGEA DC

Tarehe ya Kuwekwa: January 6th, 2026


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abasi Ahmed, leo Januari 6, 2026, amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ambapo amekagua utekelezaji wa miradi mitatu ya maendeleo katika sekta ya elimu inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Ziara hiyo imelenga kutathmini maendeleo ya miradi, ubora wa ujenzi pamoja na matumizi ya fedha za Serikali na wadau wa maendeleo.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa alianza ukaguzi wake katika Shule ya Sekondari Jenista Mhagama, ambako alikagua ujenzi wa mabweni mawili, madarasa sita pamoja na matundu kumi ya vyoo. Ujenzi wa miundombinu hiyo unagharimu jumla ya shilingi milioni 417 za Kitanzania, kwa ufadhili wa BARRIC ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Aidha, ukaguzi uliendelea katika Shule ya Sekondari Amali Lundusi, ambapo Mkuu wa Mkoa alikagua ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo jengo la utawala, vyoo vya wavulana na wasichana matundu 6, madarasa nane, nyumba ya mwalimu, maktaba pamoja na jengo la TEHAMA. Miradi hiyo kwa pamoja inagharimu jumla ya shilingi milioni mia tano na hamsini, huku shule hiyo ikiwa katika hatua ya mwisho ya ukamilishaji wa ujenzi.

Ziara hiyo ilihitimishwa katika Shule ya Msingi Mnyonga, ambako alikagua ukarabati wa madarasa yaliyopo, ujenzi wa madarasa mapya pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo. Miradi hiyo, inagharimu takribani shilingi milioni 132 kwa ufadhili wa programu za BOOST pamoja na SWASH.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Brigedia Jenerali Ahmed Abasi Ahmed alisema kuwa Serikali inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo yenye matokeo chanya yanayoonekana moja kwa moja kwa wananchi, huku matokeo yake yakionekana wazi katika Mkoa wa Ruvuma, hususan katika sekta ya elimu. Hivyo aliwataka wasimamizi wa miradi hiyo kuharakisha miradi hiyo ili iweze kutumika kwa mapema iwezekanavyo

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mheshimiwa George Ponera, kwa niaba ya wataalamu wa Halmashauri hiyo, alipokea maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa na kuahidi kuyatekeleza kwa ufanisi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • PPRA KANDA YA KUSINI YATOA MAFUNZO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KWA WATUMISHI SONGEA DC

    January 13, 2026
  • MAAGIZO 10 YA NAIBU WAZIRI KWAGILA; WATAALAM WATAKIWA KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA MIRADI

    January 11, 2026
  • WADAU SONGEA WAPEWA ELIMU YA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 09, 2026
  • MWAMPAMBA AIPONGEZA SONGEA DC NA KUSISITIZA MIKOPO YA 10% IENDELEE KUTOLEWA.

    January 08, 2026
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa