• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RC MNDEME atoa maagizo kwa watendaji Serikalini

Tarehe ya Kuwekwa: April 15th, 2021

Mkuu wa mkoa Ruvuma Chistina Mndeme amewaagiza wakuu wa Taasisi serikalini kusikiliza na kutatua kero za wananchi kuanzia ngazi ya chini.

Mndeme ametoa kauli hiyo katika kikao cha kazi cha watendaji na wakuu wote wa Taasisi za serikali mkoani Ruvuma kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa Songea.

“Mimi kama Mkuu wa Mkoa nimekuwa nikipokea kero mbalimbali ambazo wakati mwingine kero hizo zingetatuliwa katika ngazi ya wilaya au kijiji,nimeona ni vema niwaite wakuu wa Taasisi zote, kwa sababu tunapaswa kutatua kero za wananchi kwenye maeneo yetu’’,alisisitiza.

Amewaagiza watendaji hao kusikiliza kero za wananchi kwa wakati na kuwaagiza kutosubiri kero kuwafikia ofisini badala yake waweke ratiba ya kwenda kwa wananchi kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati.

Mndeme ameagiza kila Halmashauri na Taasisi kuunda mkakati wake wa kushughulikia kero za wananchi ili kupunguza kero hizo kuanzia ngazi ya chini.

“Sasa hivi tuna tatizo la mara kwa mara la kukatika kwa umeme,wewe Meneja wa TANESCO kazi yako ni nini,watu wamelipia umeme,hawajaunganishiwa umeme,wewe kama Meneja wa TANESCO kwanini huendei kwa wananchi na kutoa sababu za kero hizo,tutoe taarifa kwanini maji yamekatika,sio mimi Mkuu wa Mkoa nikatoe taarifa kwa wananchi,tuwasiliane na wananchi’’, alisema Mndeme.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amezitaja sababu mbili kubwa zinaosababisha kero kwa wananchi ni kutokufanyika vikao vya kisheria na wananchi na kutokuwepo kwa mahusiano mazuri miongoni mwa watendaji wa serikali hivyo ameagiza kufanyika kwa vikao vya kisheria na kuimarisha mahusiano ndani ya Taasisi za serikali ambayo yatasaidia kupunguza kero kwa wananchi.

“Tukitekeleza majukumu yetu vizuri kwa wananchi,tutaifanya kazi ya Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan kuwa nyepesi,sisi ndiyo tupo chini,tutoke maofisini,tusisubiri ziara ya Mkuu wa Mkoa,ninyi wakuu wa Taasisi mnaruhusiwa kwenda kuzungumza na wananchi na kutatua kero zao’’,alisisitiza.

Mndeme ameagiza kila Taasisi kuandaa rejesta ya malalamiko ya ambayo itaratibu malalmiko pia kuunda timu ndogo itakayosaidia kuratibu malalamiko na kuyafikisha kwa mkuu wa Taasisi na kwamba kero za kisera zipelekwe ngazi ya juu ili ziweze kupata utatuzi wa kisera.

Ili kuhakikisha utatuzi wa kero unakuwa endelevu,Mkuu wa Mkoa ameziagiza Taasisi za serikali kila mwisho wa mwezi kufanya tathimini namna kero zilivyoshughulikiwa na kutoa taarifa za kero zinazohitaji ufafanuzi wa kisera kwa wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho amesema ilani ya CCM ya 2020/ 2025 inalitaja moja ya jukumu lake ni kusikiliza malalamiko ya wananchi hivyo jambo linalofanywa na uongozi wa mkoa wa Ruvuma ni utekeleza wa ilani.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro amesema katika kushughulikia malalamiko ya wananchi na kwamba hakuna mfumo wa pamoja,hali inayosababisha wananchi kutojua wakimbilie wapi katika kupata suluhu ya matatizo yao.

Ili kuhakikisha kero za wananchi zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu,Mkoa wa Ruvuma umeazimia kuunda timu ya Mkoa ya kutatua kero zinazowakabili wananchi ambayo itakutana kila baada ya miezi mitatu.

Imeandikwa na 

Jacquelen Clavery

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa