• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RC. AHMED , AONGOZA KAMATI YA MAANDALIZI YA TAMASHA LA UTAMADUNI

Tarehe ya Kuwekwa: September 5th, 2024

Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Tatu la Utamaduni na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa, ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Ahmed Abbas Ahmed, imefanya kikao muhimu katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ili kujadili mikakati ya kufanikisha matukio hayo mawili makubwa. 

Mhe. Ahmed alifungua kikao kwa kufikisha salamu za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa, "Rais wetu anafanya kazi bila kupumzika kuhakikisha miradi ya maendeleo ya wananchi inapata fedha za kutosha. Anatutaka tuhakikishe fedha hizo zinatumika vyema kukamilisha miradi kwa ajili ya ustawi wa wananchi."

Akizungumzia maandalizi ya Tamasha la Utamaduni, Mhe. Ahmed alieleza kuwa maandalizi yamefikia hatua nzuri na kuwaomba wote kushirikiana kama timu moja ili kufanikisha tukio hilo. Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi na kuomba kwa Mungu ili tamasha liende salama na kwa amani.

Katika maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa, Mkuu wa Mkoa alisisitiza umuhimu wa kuwahamasisha wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 27 Novemba. Aidha, aliwahimiza watu wenye sifa kujitokeza kugombea nafasi za uongozi ili kuhakikisha tunapata viongozi wenye uwezo wa kuleta maendeleo ya kweli.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Wilman Kapenjama Ndile, aliwakaribisha wananchi kutoka ndani na nje ya nchi kushiriki katika Tamasha hilo la kihistoria. Alisema kuwa maandalizi ya tukio hilo yanazingatia usalama na kwamba wageni watapata huduma bora za malazi na usalama. "Nawaomba mjitokeze kwa wingi kuanzia siku ya ufunguzi hadi siku ya  kilele cha Tamasha ," alisema.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Makondo, aliwasilisha taarifa ya maandalizi, akieleza kuwa kutakuwa na siku nane za maandalizi, zikiambatana na midahalo ya wanafunzi, mashindano ya ngoma za asili, maonyesho ya magari ya zamani, mdahalo wa kiutamaduni, na mashindano ya mpira wa miguu.

Wadau mbalimbali waliohudhuria kikao hicho walipongeza juhudi za kuandaa Tamasha hilo, wakisema kuwa litatoa fursa nyingi za kiuchumi na kimaendeleo. Waliomba juhudi zaidi zifanywe kuhamasisha uchangiaji wa michango kutoka kwa wadau, hususani wawekezaji, ili kufanikisha tukio hilo kwa kiwango cha juu zaidi na kuiweka Ruvuma katika ramani ya matukio makubwa ya utamaduni nchini.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KULA YAMEANZA SONGEA DC

    April 29, 2025
  • MHE . JENISTA MHAGAMA AZINDUA MADARASA 27 NA VYOO MATUNDU 44, SONGEA DC

    March 16, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa