• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

RAIS Samia atoa shilingi milioni 600 kujenga shule ya sekondari Kizuka

Tarehe ya Kuwekwa: January 8th, 2022

Serikali kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari Nchini (SEQUIP) imetoa shilingi milioni 600 kujenga shule ya sekondari katika Kijiji cha kizuka Kata ya Kizuka Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Afisa mipango wa Halmashauri hiyo Nyange Athumani amesema fedha hizo zitatolewa kwa awamu mbili  ambapo awamu ya kwanza imetoa shilingi milioni 470 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa mradi huo.

Nyange ameitaja miundombinu ambayo inaanza kujengwa kuwa ni vyumba nane vya madarasa,maabara tatu za sayansi,jengo la utawala,maktaba,chumba cha TEHAMA,vyoo vya wanafunzi matundu 10 kwa wasichana na wavulana miundombinu mingine ni tanki la maji la lita 10,000 na nguzo yake na miundombinu ya kunawa mikono na kuvuna maji.

Nyange amesema fedha za ujenzi wa shule hiyo zimeshaingizwa kwenye akaunti ya shule ya Sekondari Magagura pia taratibu za kuanza ujenzi zimemeshafanyika ikiwa na pamoja na kutambulisha mradi kwa wananchi kupitia mkutano wa hadhara na kuunda kamati zitakazo husika na usimamazi wa mradi.

Ameongeza kwakusema awamu ya pili ya ujenzi wa nyumba za walimuna ununuzi wa vifaa vya chumba cha TEHAMA ambapo serikali itatoa kiasi cha shiringi milioni 130 kwa kukamilisha miradi hiyo.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kizuka Mhe.Jakob Nditi amemshukuru Rais wa awamu ya sita Mhe Samia Suluhu Hassani kwa kuwapatia fedha wananchi wa Kata ya Kizuka za ujenzi wa shule ya sekondari ambayo inakwenda kutatua changamoto ya wanafunzi kutembea umbali umrefu kufuata masomo katika shule sekondari ya Magagura.

Mhe. Nditi amesema wananchi wa Kata hiyo wameshatoa eneo lenye ukubwa wa ekeri 35 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo na wapo tayari kushirikiana bega kwa bega na wataalam katika kufanikisha ujenzi wa mradi huo.

Wamesema kukamilika kwa ujenzi wa mradi huo kutasaidi kuongeza ari ya  watoto wao kusoma na  kutotembea umbali mrefu kufuata masomo katika shule ya sekondari ya Magagura.

Mradi wa SEQUIP unalenga kuongeza fursa ya upatikanaji wa elimu ya Sekondari ,kuweka mazingira salama ya elimu kwa wasichana na kuhakikisha wanafunzi wote wanapata elimu bora ya sekondari.

Kujengwa kwa shule hiyo kunafikisha idadi ya shule 17 za sekondari zinazomilikiwa na Serikali kwa kata zote 16 za Halmashauri hiyo na kuondoa changamoto ya upungufu wa shule za sekondari kwa sasa.

Imeandaliwa na kuandikwa na

Jacquelen Clavery

Afisa Habari 

Songea DC   

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa