• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Naibu Waziri aagiza Maafisa wa Maendeleo ya Jamii kusimamia stahiki za wanawake

Tarehe ya Kuwekwa: August 12th, 2021

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto Mhe. Mwanaidi Hamis Ali amewaagiza Maafisa wa maendeleo ya jamii kusimami stahiki za wanawake zinazojuisha umiliki wa mali ili waweze kujikwamua kiuchumi.

 Mhe. Ali ametoa maagizo hayo alipofanya ziara ya kutembelea kikundi cha  wajasiriamali wadogo cha Ukombozi kilichopo Kijiji cha Peramiho Kata ya Peramiho ,Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma hivi karibuni.

Mhe.Ali amesema katika dhana ya wanawake kujikwamua kiuchumi bado kunachangamoto ambazo zimekuwa zikikwamisha jitihada za wanawake kushindwa kumiliki mali ikiwemo ardhi na nyumba kutokana na mitizamo hasi ya kwenye jamii.

Mhe Ali amevitaja baadhi ya vitendo ambavyo vimekuwa vikukwamisha jitihada hizo kuwa ni ukatili wa kijinsia,dhuluma, udhalilishaji,ubaguzi na mila potofu ambazo zinamkandamiza mwanamke katika kumiliki mali na kuendelea kuonekana kuwa dhaifu kwenye jamii.

Ameongeza kwakusema uwezeshwaji wa wanawake kiuchumi utasaidi kuleta usawa na ustawi wa jamii lakini bado kundi kubwa la wanawake wanaonekana kubaki nyuma na kuonekana kuwa dhaifu katika kujikwamua kiuchumi.

“Nawaagiza Maafisa maendeleo ya jamii kuongeza kasi ya kuhamasiha jamii kujiunga na vikundi vya kiuchumi na kutoa elimu ya ujasiriamali ili Serikali iweze kuwapa mikopo yenye masharti nafuu kupitia mifuko ya uwezeshaji ya wananchi kiuchumi”,amesisitiza Mhe Ali.

Amewahimaza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuendelea kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwaajili ya kuwawezesha wanawake kuimarisha vikundi vyao vya kiuchumi kwasababu swala hilo lipo kisheria.

Amewataka wanawake kuzingatia taratibu za kukopa na kurejesha mikopo wanayo kopa ili kutoa fursa kwa wengine kuweza kukopa na kunufaika na mikopo hiyo.

Amewarai wazazi na walezi kuendelea kutoa elimu ya malezi kwa watoto wao kitendo ambacho kitasaidia kujenga uelewa kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia na kulinda maadili katika jamii,pamoja na wanawake kuachanana tabia ya kukumbatia matatizo ya ukatili wa kijinsia badala yake wayafikishe kwenye vyombo vya kisheria ili haki iweze kutendeka.

Kwaupande wao wanawake hao wamesema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo malighafi wazotumia kutengenezea bidhaa zao kuwa bei ghari,uhaba wa masoko na mikopo ya asilimia 10 iliyotengwa na Serikali kuwa ni ndogo.

Naye Kaimu Afisa maendeleo ya jamii wa halmashauri ya wilaya ya songea Zawadi Nyoni amesema  kwa kipindi cha mwaka wa fedha cha 2019 hadi 2021 Halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo kwa vikundi 22 wenye thamani ya Tsh milioni 82.

Halmashauri ya Wilaya ya songea inazaidi ya vikundi 100 vilivyosajiliw vikijumuisha wanawake,Vijana na Walemavu.

Imeandaliwa na kuandikwa na

 Jacquelen Clavery

Afisa Habari

Songea Dc

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa