• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

UZINDUZI wa Jukwaa la wadau wa usimamizi na uendelezaji wa Rasilimali za Maji

Tarehe ya Kuwekwa: December 1st, 2020

MKOA wa Ruvuma umezindua Jukwaa la wadau wa Usimamizi  na uendelezaji wa Rasilimali za Maji katika Dakio la sehemu ya juu ya mto Ruvuma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme. 

Uzinduzi huo umefanywa na Katibu Tawala Msaidizi Jeremia Sendoro  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Chistina Mndeme uliofanyika   katika ukumbi wa Chuo cha VETA Mjini Songea Mkoani Ruvuma.

Sendoro amesema ni fursa kwa wadau kujadili na kutoa maoni na mapendekezo ya namna ya kutunza vyanzo vya maji ili visiharibiwe.

Sendoro amesema kwa upande wa  Serikali ya Mkoa wa Ruvuma imejipanga, wananchi wanaoishi sehemu ya mradi huu  itahakikisha unatekelezwa,nakuunda  jumuiya ya watumia maji, sheria za vijiji na Halmashauri ambazo zitalinda watumia maji wote ili asiwepo mtu wa kukosa maji au kupata maji kidogo kulingana na Mahitaji isipokuwa wote wafuate sheria zilizowekwa.

“Tutatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri,watendaji wa Kata na Makatibu Tarafa na viongozi wote  kuhakikisha wanatekeleza maazimio haya     kwamba wananchi wa Ruvuma  wanapata  Maji na yasichafuliwe wala kupotea bila utaratibu, maji haya tumeyalithi kutoka vizazi vilivyopita nasi tuwalithishe vizazi vijavyo”.alisema Sendoro

Amesema usimamizi na utunzaji wa Rasilimali za Maji kwa mfumo wa mabonde  unasimamiwa na Sheria ya Maji na11 ya mwaka 2009 kusimamia,kupanga,kuendeleza na kutunza Rasilimali za Maji nchi imegawanyika  katika mabonde 9.

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Ruvuma na Pwani ya kusini  Sudi Mpemba amesema anao wajibu wa kusimamia rasilimali za  Maji katika mabonde na utaratibu waliouanzisha  wa kuzindua  Majukwaa ya Mabonde na  kusimamia Maji umeanza ngazi ya Taifa ni mwongozo wa sera ya mwaka 2002.

Amesema kutakuwa na mwongozo unaelekeza kusimamia Maji ngazi ya Taifa na na ngazi inayoifuata ni Madakio na ndiomana leo tumekutana na wadau kuzindua Jukwaa la  usimamizi wa rasilimali za maji sehemu ya dakio la Mto Ruvuma kwa watumiaji wa sehemu ya juu ndiko kwenye chanzo cha maji sehemu ya matogoro na wanatumia Wilaya ya Mbinga,Songea,Nyasa na Namtumbo

Hata hivyo amesema kupitia jukwaa hili nikuwafanya wadau waweze kuzungumza namna bora ya kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji bonde la Maji na kuangalia  changamoto pamoja na kutatua Migogoro .

“Tunatambua watumia maji wapo wa aina mbalimbali kutoka kwenye mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali mfano shamba la kahawa Avivu,watumiaji wanaozalisha umeme,pia kuna wadau wa Halmashauri ya  Mbinga, Nyasa na  tupo hapa kuunda vikundi kwaajili ya usimamizi na tayari umeainisha kwenye mpango wa  usimamizi  na umekamilika na unahitaji kutekelezwa”.amesema mpemba

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya watumia Maji Bonde la Ndanda Andrew Mwanjela amesema Kwa Mkoa wa Mtwara wamejipanga lakini wanapata changamoto ya uelewa wa  wananchi ni mdogo kwamba chanzo cha maji ni nini? na kutoa visingizio vya Elimu wakati wataalamu wanatoa kila mara,amesisitiza kupitia Jukwaa hili maamuzi yatolewe ili kulinda vyanzo vya maji na kuepuka uhaba wa Maji.

Imeandikwa

Jacquelen Clavery

Songea DC

Desemba 1,2020.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa