• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Awasihi Maafisa Kilimo Kuongeza Tija Kwa Kutumia VishikwambI

Tarehe ya Kuwekwa: November 11th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Bi Elizabeth Gumbo amegawa vishikwambi kwa Maafisa Ugani Kilimo wa Halmashauri hiyo kama sehemu ya mkakati wa serikali wa kuboresha sekta ya kilimo nchini Tanzania.


Akiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa hivyo, Bi Gumbo alisema kuwa serikali imekuwa mstari wa mbele kuwekeza katika sekta ya kilimo kwa kutoa vifaa muhimu kama pikipiki, raincoat, viatu, na vifaa vya kupima udongo, ambavyo vitasaidia maafisa kilimo kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. "Hii ni sehemu ya dhamira ya serikali kuhakikisha maafisa kilimo wanawafikia wakulima kwa urahisi, wakitoa ushauri wa kitaalamu na kusaidia kuimarisha uzalishaji wa mazao," alieleza.


Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa lengo la serikali ni kuwasaidia wananchi kuboresha kipato kupitia kilimo na kuwawezesha kuondokana na umasikini. Alisema kuwa vishikwambi hivi vimesajiliwa rasmi na vimeunganishwa na mifumo ya taarifa za kitaifa ili kuwezesha ufuatiliaji wa taarifa za wakulima katika ngazi zote. "Vishikwambi hivi vitawawezesha maafisa kilimo kusajili wakulima, kutuma taarifa zao kwa urahisi, na kusaidia kufuatilia maendeleo ya shughuli za kilimo hadi makao makuu."


Aidha, aliwahimiza maafisa Ugani kilimo kutumia vifaa hivyo kwa uadilifu na kuacha tabia ya kuvifungia ndani. Alisisitiza kuwa vifaa hivyo ni mali ya umma na vinapaswa kutumika kwa manufaa ya wananchi. “Tusije tukafunga vifaa hivi ndani na kuendelea na shughuli zetu binafsi. Maafisa kilimo wana wajibu wa kwenda kwa wananchi na kuhakikisha vifaa hivi vinatumika kuongeza tija katika sekta ya kilimo ambayo ni tegemeo kubwa kwa Halmashauri yetu,” aliongeza.


Kwa hatua hii ya kugawa vishikwambi na vifaa vingine muhimu, serikali imeonesha dhamira ya dhati ya kuinua hali za wananchi kupitia sekta ya kilimo. Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa wataalamu wa kilimo wanapata rasilimali wanazohitaji ili kuwasaidia wakulima kuongeza uzalishaji, kuongeza kipato na hatimaye kuboresha maisha yao.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa