• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA ATANGAZA RASMI SHULE ZIMEFUNGULIWA WATOTO WAKASOME

Tarehe ya Kuwekwa: January 9th, 2024


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Ndg Neema M Maghembe amesisitiza wazazi na walezi wote wenye watoto wanaotakiwa kuanza masomo wahakikishe wanapelekwa shuleni kuanza kusoma ili kuendana na kalenda ya masomo ya mwaka 2024.

Ameyazungumza hayo wakati akitoa taarifa rasmi ya kufunguliwa kwa shule zote za Serikali katika Halmashuri ya Wilaya ya Songea na Tanzania kwa ujumla ambapo shule zote za msingi na sekondari zimefunguliwa rasmi 08 January 2024, hivyo Mkurugenzi Mtendaji amesema wanafunzi hao wanaotakiwa kuwasili shuleni kwani mazingira ni wezeshi kwa kila mwanafunzi kujifunza. Amesema 

"Halmashuri ya Wilaya ya Songea ina jumla ya shule ya za msingi takribani 80 na zote zinapokea wanafunzi wa Darasa la awali na Darasa la kwanza hivyo nitoe wito kwa wazazi wote ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea kumpeleka mtoto shuleni mapema ili akaanze masomo, wala mzazi asigope kama hana sare kwani Serikali imeweka utaratibu mzuri wanafunzi wote watapokelewa bila kujali kama ana sare ya shule au Hana sare ya shule"

Vilevile Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuongeza shule katika Halmashuri ya Wilaya ya Songea hasa katika maeneo ambayo shule zilikuwa na msongamano mkubwa wa wanafunzi kwa mfano shule ya msingi Nambarapi Kata ya Kilagano, shule ya msingi Jenista iliyopo Kata ya Muhukuru, pia Shule ya sekondari Jenista Mhagama iliyopo Kata ya Parangu hivyo kupitia shule hizi mpya zimewezesha kupunguza msongamano wa wanafunzi pia kupunguza umbali mrefu wa kutembea kwa wanafunzi, vilevile ameishukuru Serikali kwa kuweka miundombinu mizuri katika shule hizo ikiwemo madawati. Hivyo amewatoa hofu wanafunzi wote ambao wanaotakiwa kuanza masomo waende wakasome kwa kuwa kuna mazingira wezeshi.

Nao baadhi ya wanafunzi wa Shule za msingi wametoa Shukrani kwa Serikali kwa mapokezi mazuri kwa wanafunzi wanaoanza na hata wale wanaoendelea wameishukuru Serikali kwa kuwaboreshea miundombinu ikiwemo Madarasa, madawati na viti. Wamesema

Stevia Mbunda mwanafunzi wa Darasa la sita Shule ya msingi Nambarapi " Tunamshukuru sana Mhe Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutujengea shule nzuri ina madawati, Madarasa ya kutosha nasi tunamuahidi kusoma kwa bidii"

Yakobo Mwenda mwanafunzi wa Shule ya msingi Mgazini amesema" tunawashukuru sana wazazi wetu kwa kutununulia sare za shule, wametulipia chakula nasi sasa tunakila shuleni, pia Tunamshukuru sana Serikali kwa kutulipia ada kwa upendo huo nasi tunaahidi kufaulu katika masomo yetu"

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa