• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Miti inayogeuka mawe kivutio kipya cha utalii mkoani Ruvuma

Tarehe ya Kuwekwa: December 7th, 2020


Kijiji cha Mbati kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kimebarikiwa kuwa na msitu wenye magogo yaliyogeuka mawe hali inayosababisha kutembelewa na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Mratibu wa Utalii Kanda ya Kusini ambaye pia ni Afisa Msaidizi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Wilaya ya Tunduru Debora Mwakanosya  amesema miti inayogeuka mawe (Miti mawe) ni jamii ya miti ya mitetereka ambayo duniani inapatikana nchi mbili ambazo ni Marekani na Tanzania.

“Kwa Tanzania miti mawe inapatikana Mkoa wa Ruvuma  katika kijiji cha Mbati wilaya ya Tunduru,pia miti hiyo inapatikana katika Wilaya ya Namtumbo eneo la Likuyu Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na katika pori la Akiba la Liparamba wilaya ya Nyasa’’,alisema.

Amesema mti huo ukiuona juu kabla ya kugeuka jiwe unakuwa ni mti wa kawaida na kwamba mti huo unageuka jiwe kutokana na mfumo wa asili ambao Mungu ameutengeneza kwa kuwa mti huo unageuka jiwe zito kabisa.

Amesema kivutio hicho cha miti mawe kinaufanya utalii wa Mkoa wa Ruvuma kuwa ni wa kipekee na tofauti kabisa na kwamba aina hiyo ya miti ina uwezo wa kudumu zaidi ya miaka 120.

Hata hivyo Mtaalamu huyo wa miti amesema miti hiyo ipo katika hatari kubwa ya kutoweka kutokana  na watu wengi kuikata kwa matumizi mbalimbali,ambapo amesisitiza miti hiyo inatakiwa kuhifadhiwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Naye Sandali  Mtenje Mzee maarufu katika kijiji cha Mbati chenye  msitu wenye magogo yaliyogeuka mawe,amesema aliona vipande vya mti uliogeuka mawe tangu mwaka 1983 na kwamba miaka hiyo vipande hivyo vya magogo vilikuwa katika hatua za awali za kugeuka mawe.

Sandali anasema miaka tisini waliona wageni wengi wanatembelea mara kwa mara msitu wa kijiji hicho wakiwemo raia wa kigeni ambao walifika kuona miti hiyo ikiwa imegeuka mawe.

“Baada ya muda tukagundua wazungu wanafika hapa tena bila hata kuona viongozi wa kijiji wanapandua magamba ya miti hiyo na wengine wanachukua vipande vya miti iliyogeuka mawe na kuondoka navyo’’,alisema Sandali.

Utafiti uliofanywa katika pori la akiba Selous ambalo sasa ni hifadhi ya Taifa ya Nyerere  na wataalam kutoka nje ya nchi kwa kushirikiana na wataalam wa Wizara ya Maliasili na Utalii umebaini kupatikana zaidi ya aina(species) 2100 za mimea zilizotambuliwa na wanasayansi ikiwemo aina 600 za miti ambayo haipatikani sehemu nyingine duniani.

Mkurugenzi Mstaafu wa Uhifadhi ambaye pia amewahi kuwa Mkuu wa Chuo cha Wanyamapori Likuyuseka Namtumbo  Ngwatura Ndunguru anaitaja Moja ya  jamii ya miti ambayo haijafahamika na kutangazwa ipasavyo  kuwa ni  magogo ya miti iliyogeuka mawe jamii ya miti ya mitetereka ambayo kitaalam inaitwa fossilized tree trucks .

Amesema masalio ya magogo  hayo  bado yanaonekana katika baadhi ya maeneo ya ndani hifadhi ya Selous(Hifadhi ya Taifa ya Nyerere) na  katika vijiji vya Mpurakacheche na Mbarang’andu Wilaya ya Namtumbo Mkoa wa Ruvuma.

Ngwatura anasisitiza kuwa miti mawe hiyo ikitangazwa kwenye vyombo vya habari,mamia ya watalii wanaweza  kufika katika Mkoa wa Ruvuma na kuona kivutio hicho kipya na cha kipekee  hivyo  kuingiza mapato na fedha za kigeni ambazo zitasaidia kuinua uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake Afisa Utalii wa Pori la akiba Liparamba wilayani Nyasa Maajabu  Mbogo amesema miti mawe inapatikana kwa wingi katika eneo la Nakatuta ndani ya hifadhi hiyo.

Kwa mujibu wa Mhifadhi huyo,maeneo yote ambayo miti imegeuka mawe hayakaliwi na watu wengi wala hakuna mtu anayeingia ndani ya eneo hilo hali iliyosababisha maeneo hayo kubakia katika hali yake ya asili ya kijiolojia ya kutoharibiwa kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Desemba 7,2020

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa