• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MILIONI 311 ZATENGWA UJENZI WA SHULE MPYA YA AWALI NA MSINGI KATIKA KIJIJI CHA MAGAGULA,

Tarehe ya Kuwekwa: August 25th, 2025


Agosti 24, Kaimu Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndugu Solteri Nchimbi, kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Halmashauri hiyo, wametambulisha rasmi mradi wa ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi katika kijiji cha Magagula, Shule hiyo itakayojengwa katika eneo la shule ya sekondari Magagula inatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi milioni 311.

Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara, Nchimbi alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo ni sehemu ya mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kukuza elimu kwa watoto wa Tanzania. Alisisitiza ushirikiano wa wananchi katika utekelezaji wa mradi huo, akieleza kuwa shule hiyo inatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika ifikapo Januari 2026.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Mipango wa Halmashauri hiyo, Bi Sylvia Festo, aliwahimiza wananchi kushirikiana kwa karibu na kamati ya ujenzi pamoja na wataalamu wa Halmashauri. Alisema wananchi wanapaswa kufuatilia maendeleo ya mradi huo na kutoa taarifa pindi changamoto zitakapojitokeza ili kupatiwa ufumbuzi mapema.

Naye Afisa Manunuzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Ndug Raymond Aloyce, alisisitiza kamati ya ujenzi kuzingatia sheria na taratibu za manunuzi kupitia mfumo wa kidijitali wa NeST, ambao unaweka wazi mchakato mzima wa manunuzi. Aidha, alibainisha kuwa hata mafundi wanaotarajiwa kushiriki katika ujenzi huo watapaswa kuomba kupitia mfumo huo kwa kuzingatia vigezo husika.

Kwa upande mwingine, Mhandisi Hafidhi Kimaro kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songea alikumbusha wajibu wa kuzingatia BOQ (Bill of Quantities) zilizopangwa, ili kuhakikisha ujenzi unakuwa wa kiwango bora na wenye tija kwa vizazi vinavyotarajiwa kunufaika na shule hiyo.

Pia katika mkutano huo wananchi waliweza kuunda kamati ya ujenzi wa Mradi huo ili kufanikisha mradi. Mradi huo unatarajia kujumuisha ujenzi wa miundombinu muhimu ikiwemo madarasa, ofisi pamoja na vyoo, hatua itakayosaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa kijiji cha Magagula na maeneo jirani.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa